Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ESTHER E. MALLEKO) aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kufufua Kiwanda cha Magunia Moshi Mkoani Kilimanjaro ili kukuza ajira na uchumi kwa wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa kwenye jibu la msingi Naibu Waziri amesema kwamba magunia ya katani ni ya adimu na yanahitajika sana; na kwa kuwa Mkoani Kilimanjaro ikiwemo Same, Mwanga ni wakulima wazuri wa katani lakini katani hiyo haipati namna ya kuhifadhiwa. Je, ni kwa nini Serikali haioni uharaka sasa kuzungumza na Mohamed Enterprise ambaye pia alimiliki mashamba hayo na akamiliki kile kiwanda ili waweze kutengeneza magunia? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ametutajia kuwa kuna viwanda nane na vitatu ndiyo vipo active lakini magunia haya yanatumika kwenye kuweka kahawa na Mkoa wa Kilimanjaro unalima kahawa na magunia wanaagiza kutoka nje. Je, Serikali inasema nini kuhusu hilo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shally Raymond, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema ni kweli kuna changamoto katika zao la mkonge kwa maana ya uchakataji. Sasa hivi Serikali inafanya juhudi kwanza kuongeza uzalishaji wa mkonge kwa maana ya malighafi, lakini pia kuhakikisha wazalishaji kwa maana ya wachakataji kwenye viwanda wanaendelea. Ndiyo maana tumesema moja ya kazi tunazozifanya ni kuwapa vivutio maalumu ikiwemo kuwalinda wazalishaji wa ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimueleze tu Mheshimiwa Shally Raymond kwamba huyu mwekezaji METL kwa maana Mohamed Enterprise tayari tumeshaanza kumpa baadhi ya mikataba kwa ajili ya kuzalisha vifungashio kwa maana ya magunia hayo katika zao la korosho. Hii ni mojawapo ya mipango ambayo tunadhani kwa sababu ana uhakika wa soko maana yake atapata mtaji na kuendelea kuzalisha kwenye viwanda hivyo vingine. Kiwanda cha Morogoro tayari kinazalisha tunaamini ataendelea kuzalisha pia katika kiwanda hicho cha Moshi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili, kama ambavyo nimesema tumeshaanza kuwapa vivutio maalum ikiwemo kuwapunguzia baadhi ya kodi kwa magunia haya ambayo yanaenda kufanya kazi kwenye vifungashio katika mazao ya kilimo. Kwa hiyo, ameanza na korosho tunaamini akiendelea kuzalisha sasa ataenda kwenye vifungashio kwa ajili ya zao la kahawa na mazao mengine. Nakushukuru.

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ESTHER E. MALLEKO) aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kufufua Kiwanda cha Magunia Moshi Mkoani Kilimanjaro ili kukuza ajira na uchumi kwa wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kupata nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa kwenye Jimbo la Same Mashariki, Kata ya Ndungu pamoja na Kata ya Mahore kuna mashamba makubwa ya kilimo cha mkonge lakini anayemiliki mashamba hayo haonyeshi kujali zao lile.

Je, Serikali mnasema nini katika hilo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anne Kilango Malecela Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema moja ya mikakati ya Serikali ni kujihakikishia kuwa tuna malighafi za kutosha ambazo zitaenda kuchakatwa kwenye viwanda vyetu ambavyo tunavihamasisha kuanza kuvifufa sasa.

Kwa hiyo, moja ya mikakati ambayo tumeshaweka kupitia Wizara ya Kilimo ni kuwapa mikakati au kuhakikisha hawa wakulima wanaendeleza sasa haya mashamba ya mkonge.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo hata hawa wa Same nakuahidi na Wabunge wapo hapa tunaendelea kujadiliana nao lakini kuhakikisha wanaenda kufufua mashamba hayo ili aweze kutoa raw material au malighafi kwenye viwanda ambavyo tunaendelea kuvifufua.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.