Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 7 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 85 2021-09-08

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SHALLY J. RAYMOND K.n.y. MHE. ESTHER E. MALLEKO) aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kufufua Kiwanda cha Magunia Moshi Mkoani Kilimanjaro ili kukuza ajira na uchumi kwa wananchi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, magunia yanayotokana na zao la mkonge ni moja ya vifungashio muhimu vya mazao ya kilimo hapa nchini. Tanzania ina viwanda nane vinavyoongeza thamani zao la mkonge. Kati ya viwanda hivyo, viwanda vitatu 3 ni vya kuzalisha magunia ya mkonge.

Mheshimiwa Naibu Spika, Kiwanda cha Magunia cha Moshi (Tanzania Bag Corporation – TBCL) kilibinafsishwa na Serikali kwa kampuni ya Mohamed Enterprise Tanzania Limited (METL). Hata hivyo, kutokana na changamoto mbalimbali kiwanda hiki kimeshindwa kuzalisha na kujiendesha kibiashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, changamoto za viwanda vya magunia ya mkonge ni mtambuka na Serikali inazishughulikia kiujumla kwa tasnia yote ya mkonge. Wizara ya Viwanda na Biashara kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo na Wizara ya Fedha na Mipango na Taasisi zake inaendelea kuchukua hatua mbalimbali za utatuzi wa changamoto ikiwemo kulinda wazalishaji wa ndani na kuwatengenezea mazingira bora ya ufanyaji biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni matumaini ya Serikali kuwa jitihada hizi zinazoendelea zitakuwa ni chachu ya kuinua kilimo cha mkonge na ufufuaji wa viwanda vya magunia ya mkonge kikiwepo kiwanda cha magunia cha Moshi na hivyo kukuza ajira na uchumi wa wananchi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.