Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - (a) Je, ni wakulima wangapi wadogo wadogo wamepata mikopo kutoka Benki ya Kilimo ili kukuza tija kwa wakulima hao? (b) Je, riba za Benki ya Kilimo zinatofauti gani na riba za Benki za Biashara katika kumsaidia mkulima mdogo?

Supplementary Question 1

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri lakini bado nina maswali ya nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, je, Serikali inaweza kutoa ruzuku ambayo zamani ilikuwa ikitoa kwa wakulima kwa mazao mbalimbali sasa iende kwenye Benki ya Kilimo halafu benki isimamie na kutoa mikopo hiyo kwa riba ndogo sana? Kilimo hakiwezi kukopeshwa zaidi ya asilimia 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, hivi karibuni Benki Kuu imetangaza fedha za kusisimua uchumi trilioni moja.

Je, haiwezekani Benki Kuu ikapeleka sehemu ya fedha hiyo kwenye Benki ya Kilimo ili yenyewe isimamie kwa kuwakopesha wakulima kwa riba ndogo? (Makofi)

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Almas Maige kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na ruzuku ya shilingi trilioni 1 ambayo urejeshaji wake utakuwa ni wa riba asilimia 3 ni mkakati maalumu ikiwa ni moja kati ya hatua tano ambazo BoT imeziweka kwa ajili ya mabenki yote nchini. Kwa hiyo, TADB ni moja kati ya mabenki ambayo yanapaswa kutumia fursa hiyo. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba TADB ni miongoni mwa mabenki kadhaa ambayo tayari yameshapeleka maombi hayo kwa ajili ya kupatiwa fedha hizo kwa ajili ya kutekeleza malengo na mikakati yake ikiwemo dhima kubwa ya kutekeleza maelekezo ya Mheshimiwa Rais kuhakikisha kwamba riba zinapungua kwa kiwango kisichozidi asilimia 10.

Mheshimiwa Naibu Spika, sambamba na hilo, kuna jitihada mbalimbali ambazo kama Serikali inachukua za kuhakikisha kwamba tunaiongezea uwezo TADB pamoja na benki nyingine zilizo chini ya mamlaka ya Serikali ili ziweze kupata mitaji ya kutosha pamoja na zenyewe kuwa na utaratibu wa kubuni njia za kujiwezesha kuongeza ukwasi ili waweze kutoa mikopo zaidi na kusaidia sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi pamoja na sekta nyingine mbalimbali nchini.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ATHUMAN A. MAIGE aliuliza: - (a) Je, ni wakulima wangapi wadogo wadogo wamepata mikopo kutoka Benki ya Kilimo ili kukuza tija kwa wakulima hao? (b) Je, riba za Benki ya Kilimo zinatofauti gani na riba za Benki za Biashara katika kumsaidia mkulima mdogo?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, Benki hii ya Kilimo ipo Dar es Salaam lakini wakulima walio wengi wapo katika mikoa mbalimbali kwa maana ya Nyanda za Juu Kusini, Mikoa ya Kaskazini na kwingineko. Je, ni lini sasa huduma hizo zitapanuka ili wakulima wote waweze kupata huduma hiyo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecilia Paresso, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Cecilia Paresso amezungumza hoja ya msingi, nimhakikishie kwamba kwa kipindi hiki ambacho TADB haijawa na matawi katika maeneo yote nchini imekuwa ikifanya kazi zake kwa utaratibu mzuri wa kuwasaidia wakulima kwa kuweka utaratibu maalumu wa kuratibu kupitia Idara Maalumu ambayo inajihusisha na masuala ya wakulima wadogo wadogo katika benki hiyo. Hata hivyo, kwa kuwa wazo hili ni jambo jema, nimhakikishie kwamba tumelipokea na tutalifanyia kazi. Pale ambapo hali itaruhusu tutaweza kusambaza huduma ya TADB katika maeneo mbalimbali nchini.