Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasha umeme kwenye Vijiji na Vitongoji vyote katika Jimbo la Arumeru Mashariki ambavyo umeme bado haujawashwa?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru tena kwa kunipa nafasi. Kwanza niseme naishukuru sana Serikali na kuipongeza kwa kazi nzuri ambayo inafanya kwa kuhakikisha kwamba inawasha umeme kwa vijiji vyote na vitongoji nchi nzima. Hata hivyo, hivi karibuni tulipata orodha ya wakandarasi ambao wamekuja kwa ajili ya kufanya kazi ya kumalizia zoezi la kuwasha umeme REA III.

Mheshimiwa Naibu Spika, kule Arusha Mkoani amekuja kandarasi mmoja tu na kule Longido, nakuwa na mashaka kwamba ahadi ya Serikali kwamba mwaka kesho watakuwa wametimiza ahadi yao ya vijiji vyote nchi nzima kuwa vimeshapata umeme; nakuwa na mashaka kwamba tutaweza kufanikisha hilo zoezi. Swali langu, je, wana mpango gani wa kuhakikisha kwamba wanaongeza idadi ya wakandarasi ili hiyo kazi na ahadi ya Serikali iwe ya kweli? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimshukuru kwa kutambua juhudi za Serikali za kuendelea kuwahudumia watanzania kwa kuwapelekea umeme katika maeneo yao na ni commitment ya Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwamba kufikia Disemba, 2022, tutakuwa tumekamilisha upelekaji wa umeme katika maeneo yote.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli wiki kama mbili zilizopita Mradi wa REA III, round II, ulizinduliwa rasmi na Mheshimiwa Waziri katika eneo la Longido na mkandarasi anayefanya kazi katika Mkoa wetu wa Arusha anaitwa SAGEMCOM na yuko kazini tayari na alikuwa amepewa maeneo matatu ya Longido, Karatu na Monduli.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na upana wa Mkoa wa Arusha, Wizara imeona ni vema kuongeza mkandarasi mwingine, aende akafanye kazi katika Jimbo la Arumeru Mashariki, Mgharibi lakini pia na Ngorongoro. Kabla ya mwezi Julai haujaisha mkandarasi atakuwa ameripoti kazini kwa ajili ya kuendelea kufanya kazi ili ile ahadi iliyotolewa na Serikali ya kufikisha umeme kwa wananchi wote ifikapo Disemba mwakani iwe imekamilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nitumie nafasi hii kuwaomba Waheshimiwa Wabunge kwa sababu baada ya hapa tunatawanyika kwenda kwenye maeneo yetu basi wakawe mkono wa kwanza kabisa wa kushirikiana na
wakandarasi kutimiza azma ya kupeleka umeme kwa wananchi kwa kuwasimamia kwa karibu na kuwa pamoja na sisi ili kuweza kufikisha hiyo ahadi. Nashukuru.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasha umeme kwenye Vijiji na Vitongoji vyote katika Jimbo la Arumeru Mashariki ambavyo umeme bado haujawashwa?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Katika awamu hii ya REA kila kijiji kimepewa kilomita moja, nataka nifahamu hizi kilomita moja zinaanza kuhesabiwa wapi, ndani ya kijiji au nje kwa sababu kuna vijiji vingine vimeachana kilomita tatu, kutoka kijiji kimoja mpaka kufika kingine? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwenisongole kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri aliyoyatoa katika swali la msingi na swali la nyongeza la Mheshimiwa Pallangyo. Vile vile nimpongeze Mheshimiwa Mwenisongole kuuliza swali la msingi ambalo kimsingi linawahusu Wabunge wote katika majimbo yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tumetoa utaratibu mkandarasi anapoingia katika kijiji angalau atumie umbali wa kilometa moja kusambaza umeme tofauti na ilivyokuwa huko zamani ambapo ilikuwa ni wateja wawili watatu wanne. Jambo la msingi hapa ni kwamba ile kilometa moja tunayoitaja ni ndani ya kijiji, sio kati ya kijiji kimoja na kingine, ndani ya kijiji akishafika. Hata hivyo, hao ni wateja wa awali, ataendelea kuunganisha wateja wengine kadri wateja wengine wanavyojitokeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge, tusifungwe na kilometa moja, kilometa moja ni wateja wa kuanzia, badala ya kufunga transformer ukaiacha bila kuwa na mteja. Nimeona nitoe ufafanuzi wa jumla ili Waheshimiwa Wabunge wawe na imani na wateja wa kwanza wanaoanza na tuwaombe wananchi jirani na wateja wa kwanza wanaunganishwa waendelee kulipia umeme hili nao waendelee kuunganishiwa umeme. Ahsante sana.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasha umeme kwenye Vijiji na Vitongoji vyote katika Jimbo la Arumeru Mashariki ambavyo umeme bado haujawashwa?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na Kisiwa kikubwa cha Ukerewe kuwa kwenye matatizo ya umeme kwa takribani wiki tatu sasa, wananchi kwenye Visiwa vidogo vya Ilugwa na Ukara wamekuwa wananunua umeme, lakini hawapelekewi token. Je, nini kauli ya Serikali juu ya changamoto hii? Nashukuru sana.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, nampongeza sana Mheshimiwa Mkundi, Mbunge wa Ukerewe. Kesi ya wananchi wa Ukerewe inafanana sana na maeneo mengi ya visiwa, ambapo wakandarasi binafsi ambao wanapeleka umeme kwa wananchi wanaozalisha, kwanza wanauza umeme kwa bei kubwa tofauti na maelekezo ya Serikali.

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, wameanza pia mchezo, wanapopeleka kwa bei ya Serikali hupeleka kwa kiwango kidogo. Naomba nitoe tamko mbele ya Mheshimiwa Mbunge wa Ukerewe na Waheshimiwa Wabunge, mara baada ya Bunge tutatembelea maeneo yote yenye kero ya namna hiyo na kutoa maelekezo kwa mameneja wetu kuwasimamia wakandarasi wa namna hiyo ili kupeleka umeme kwa bei elekekezi ya Serikali ya Sh.100 kwa unit na kuendelea kutoa umeme kwa wananchi kulingana na mikataba yao inavyowaelekeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, nitakwenda kwa Mheshimiwa Mkundi, Ukerewe. Pia nitatembelea Maisome na maeneo mengine ili kutoa maelekezo ya Serikali na namna ya kuyasimamia. Ahsante sana.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasha umeme kwenye Vijiji na Vitongoji vyote katika Jimbo la Arumeru Mashariki ambavyo umeme bado haujawashwa?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Katika Wilaya ya Karatu kuna Mji Mdogo wa Karatu, sasa huu Mradi wa REA umelenga sana kwenye vijiji na pale Mji wa Karatu wanasema ni mjini lakini ni bado vijijini sasa ni lini Serikali ina mpango gani katika ile miji midogo ambayo umeme huu wa REA haujapelekwa ili kuwasaidia wananchi wakiwemo wa Jimbo la Karatu wa Mji wa Karatu?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Daniel Awack, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli upelekaji wa umeme unaofanywa na Serikali uko katika picha na maeneo tofautitofauti; ziko hizo tunazoziita REA ambapo tumekuwa na awamu kadhaa, lakini iko miradi ya densification, inapeleka umeme kwenye vitongoji, lakini hiko miradi tunaita peri-urban.

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi ya peri urban inapeleka umeme kwenye maeneo ya miji lakini ambayo bado yana asili ya vijiji, Jimbo la Bukoba Mjini likiwemo na kwa Karatu ikiwemo, maeneo ya Mwanza yakiwemo, Geita ikiwemo, tutahakikisha kwamba kufikia mwezi Februari tumeanzisha huo mradi wa peri-urban unaoweza kupeleka umeme kwenye maeneo ambayo ni ya mijini lakini bado yana asili ya vijiji ili na sisi pia tuweze kunufaika na umeme huo.

Name

Anton Albert Mwantona

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasha umeme kwenye Vijiji na Vitongoji vyote katika Jimbo la Arumeru Mashariki ambavyo umeme bado haujawashwa?

Supplementary Question 5

MHE. ANTON A. MWANTONA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Ni nini kauli ya Serikali kwenye Jimbo letu la Rungwe kuna vijiji 24 ambavyo vilikuwa kwenye REA II havijapatiwa umeme, lakini pia kwenye REA III, round ya pili vijiji tisa haviko kwenye orodha ya kupatiwa umeme katika hii REA III, round ya pili. Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mwantona, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge kwa kuuliza swali la maeneo ambayo yalisahaulika. Tumeshatoa maelekezo na taarifa kwa Waheshimiwa Wabunge, naomba tena nirudie tu. Kwanza namshukuru Mheshimiwa Mbunge na kama kuna vijiji sita au tisa au vingapi ambavyo vilisahaulika tunaomba atuletee.

Mheshimiwa Naibu Spika, tumefanya utaratibu baada ya wiki mbili zilizopita, kupitia maeneo yote ya nchi nzima katika vijiji vilivyosahaulika na viko vingi. Kwa Mheshimiwa Lukuvi vilisahaulika vijiji viwili na maeneo mengine, tumepata vijiji 610 na vyote tumeviingiza kwenye mpango wa kutekelezwa na tuna shilingi bilioni 150 na wakandarasi tayari wameshapewa.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo niwape tu uhakikisho wananchi kupitia Bunge letu Tukufu kwamba kama kuna Mbunge yeyote, kijiji chake kimesahaulika tunaomba sana atuletee, Mradi wa REA III, round ya pili ni mradi wa kumbakumba wa vijiji vyote. Kwa hiyo niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge watuletee vijiji vyao vilivyosahaulika ili visisahaulike ili utekelezaji uende pamoja na maeneo yanayotekelezwa. Ahsante sana.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawasha umeme kwenye Vijiji na Vitongoji vyote katika Jimbo la Arumeru Mashariki ambavyo umeme bado haujawashwa?

Supplementary Question 6

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana. Swali langu pia lililenga hili ambalo limeulizwa na Mbunge wa Rungwe, lakini pia naomba basi niulize kwamba, kwa kuwa imekuwa ni tabia ya wakandarasi kuruka baadhi ya vitongoji, halafu wanapeleka sehemu ya mbele na vitongoji vingine ambavyo vimekatiwa miti yake havipewi. Je Serikali inasemaje kuhusu hili?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mlaghila kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Mbunge na tumeshaongea naye kuhusu vijiji na vitongoji vilivyorukwa. Naomba pia nitumie nafasi kupitia Bunge lako Tukufu kuwakumbusha tu wakandarasi na tumetoa maelekezo haya mara kwa mara, kwamba mradi wa vijiji ambavyo tunakwenda kuutekeleza sasa ambao pia una miradi ya vitongoji na mitaa, hauzingatii na hautarajii kuruka kitongoji chochote.

Kwa hiyo niwakumbushe wakandarasi kutoruka sio kitongoji tu kutoruka kijiji, kitongoji, kaya na nyumba, haitegemei ni aina gani ya nyumba. Nashukuru.