Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 62 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 525 2021-06-30

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawasha umeme kwenye Vijiji na Vitongoji vyote katika Jimbo la Arumeru Mashariki ambavyo umeme bado haujawashwa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa John Danielson Pallangyo, Mbunge wa Arumeru Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vyote ambavyo havijapata umeme katika katika Jimbo la Arumeru Mashariki vinapatiwa umeme kupitia Mradi wa REA awamu ya tatu, mzunguko wa pili ulioanza Mwezi Machi, 2021. Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kukamilika Mwezi Disemba, 2022. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 2.07.

Mheshimiwa Naibu Spika, vitongoji vya Jimbo la Arumeru Mashariki ambavyo havijafikiwa na umeme vitaendelea kupatiwa umeme kupitia mradi wa ujazilizi yaani densification unaotarajiwa kuanza mwezi Julai, 2021. Aidha, kazi ya kupeleka umeme katika vitongoji ni endelevu, Serikali kupitia TANESCO na REA itaendelea kupeleka umeme katika vitongoji kulingana na upatikanaji wa fedha.