Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, ni lini mradi wa ujenzi wa soko la kisasa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime wenye thamani ya shilingi bilioni 8.07 utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika nakuskuru. Mradi wa soko la Tarime ulikuwa uanze awali kama alivyosema February 2019 na wananchi wote waliokuwa na vibanda pale takriban 200 walibomolewa vibanda, kwa hiyo wamekuwa wakilipwa kwa muda huu wote, na majibu ya Serikali anasema utamalizika ndani ya miezi 12, na wametenda bilioni tatu tu, wakati mradi ni bilioni 8.07, ninependa kujua sasa hio bilioni 5.07 zinapatikana wapi ili ziweze kumalizika mradi huu ndani ya miezi 12 kama mlivyoonesha, maana yake mwaka wa fedha uko within that?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, tuliweza kukidhi tena vigezo vya kupata stendi ya kimkakati ya Galamasara, na wananchi walikuwa wametoa takribani milioni 70 tangu mwaka 2017, ningependa kujua pia stendi hii ya kimkakati ya Galamasara ni lini inaenda kuanza na kumalizika? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimwia Naibu Spika, kwanza nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko kwa juhudi zake za kuunga mkono juhudi kubwa za Mbunge wa Jimbo hilo Mheshimiwa Michael Kembaki katika kutetea wananchi wa Tarime Mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pili nimhakikishie kwamba Serikali imeweka mpango wa kuhakikisha miradi mkakati ukiwemo ujenzi wa soko la kisasa katika Mji wa Tarime unakamiliswa, na ndio maana katika mwaka wa fedha 2021/ 2022 tumetenga bilioni tatu na Serikali itaendelea kutenga fedha hizo kuhakikisha mradi huo unakamilika; pili fedha bilioni 5.07 zitawekwa kwenye mpango ujao wa fedha kuhakikisha linakamilishwa kwa wakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pili stand hii ya kimkakati pia ni miongoni mwa mipango ambao Serikali itaendelea kuitekeleza kwa awamu. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, lengo la Serikali ni kuhakikisha miradi hii inakamilika na safari ni hatua, tunaanza na hatua moja tunakwenda kukamilisha hatua nyingine, ahsante sana.