Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 61 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 511 2021-06-29

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, ni lini mradi wa ujenzi wa soko la kisasa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime wenye thamani ya shilingi bilioni 8.07 utakamilika?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji wa Tarime ilikidhi vigezo vya kupatiwa Shilingi bilioni 8.07 kwa ajili ya ujenzi wa soko la kisasa kupitia utaratibu wa Miradi ya Kimkakati mwezi Februari, 2019. Kutokana na changamoto zilizojitokeza wakati wa utekelezaji wa miradi ya kimakatati Serikali ilisitisha baadhi ya miradi ya kimkakati iliyoidhinishwa ukiwemo mradi wa ujenzi wa soko la kisasa katika Halmashauri ya Mji wa Tarime. Hata hivyo, Serikali imetoa kibali kwa Halmashauri ya Mji Tarime kuendelea na ujenzi wa Soko na katika mwaka wa fedha 2021/2022, shilingi bilioni tatu zimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa soko katika Mji wa Tarime.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Mji Tarime inatarajia kutangaza kazi ya ujenzi wa soko la kisasa mwezi Julai, 2021 na ujenzi unatarajiwa kuanza mwezi Agosti, 2021 baada ya kumpata mkandarasi. Halmashauri imejipanga kukamilisha mradi huo ndani ya miezi 12 tangu tarehe ya kusaini mkataba.