Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohamed Suleiman Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR aliuliza: - Je, ni kwa nini wananchi wa Tanzania Bara wanatozwa na polisi faini za papo kwa papo kwa kutotumia mashine za EFD wakati Polisi wa Zanzibar hawatozi faini za papo kwa papo kwa wananchi wasiotumia mashine hizo?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza nashukuru majibu ya Serikali kwa kufuatia maswali yangu haya; lakini swali langu la kwanza katika maswali yangu ya nyongeza kwamba kama kwa mujibu wa majibu aliyonipa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba inakiri kwamba Mamlaka ya kule Zanzibar pia inayo sheria yake ambayo inatambua hizi sheria za faini za papo kwa papo; je, ni kwa nini Jeshi la Polisi sasa limeshindwa kusimamia sheria hizi za papo kwa papo pale barabarani kwa kutumia hizi mashine za EFD? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili kwamba ni lini sasa Wizara ya Mambo ya Ndani itakaa na mamlaka husika za kule Zanzibar ili kuona Jeshi la Polisi zinaanza kutumia mashine hizi na ukizingatia kwamba itapunguza malalamiko ya wananchi na itapunguza masuala ya rushwa lakini pia itapunguza zile ajali ambazo zitaweza kuepukika? Nashukuru sana. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Spika, naomba ama napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Malindi Mheshimiwa Mohamed Suleiman Omar maswali yake mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, je, kwa nini Jeshi la polisi limeshindwa? Jeshi la polisi halijashindwa kusimamia taratibu, kanuni na sheria za usalama barabarani katika hili suala la kutumia mashine hizi hapa kuja jambo kidogo, Zanzibar kuna mamlaka inaitwa Mamlaka ya Usafirishaji au Mamlaka ya Usalama Barabarani ambayo ina sheria yake sheria namba saba na Bara kuna Baraza la Taifa la kusimamia usalama barabarani ambalo nalo lina sheria yake kama tulivyoeleza, lakini kama hilo halitoshi mamlaka hivi zote zina utaratibu wake na kanuni zake ambazo zinasimamia pamoja na kwamba Jeshi la Polisi ndio muhimili mkubwa ambao unasimamia mamlaka hizi.

Kwa hiyo, haijashindwa kusimamia tatizo lililokuwepo ni changamoto ya sheria kwamba hawa wanasheria yao, wana kanuni yao, hawa wana mamlaka yao pamoja na kwamba Jeshi la polisi ndio hilo. Kwa hiyo jeshi la polisi halijashindwa kusimamia sheria hii.

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili; je, ni lini sasa Serikali hasa kule Zanzibar itaruhusu matumizi ya hizi mashine? Nimwambie tu kwamba kwa kuwa sheria ipo na mamlaka inayosimamia usalama barabarani ipo na sheria yake ipo kikubwa ni kwamba sasa hivi tupo katika harakati za kukamilisha kanuni itakayokuja kusimamia sheria hizi ili sasa hii sheria ya kutumia hizo mashine kwa ajili ya kukinga hizo ajali na mambo mengine zianze kutumika.

Mheshimiwa Spika, kubwa nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo sana ili tumalize hizo kanuni na sheria zianze kutumika kote kote.