Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 508 2021-06-28

Name

Mohamed Suleiman Omar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malindi

Primary Question

MHE. MOHAMED SULEIMAN OMAR aliuliza: -

Je, ni kwa nini wananchi wa Tanzania Bara wanatozwa na polisi faini za papo kwa papo kwa kutotumia mashine za EFD wakati Polisi wa Zanzibar hawatozi faini za papo kwa papo kwa wananchi wasiotumia mashine hizo?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Suleiman Omar, Mbunge wa Jimbo la Malindi kutoka Mkoa wa Mjini Zanzibar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sheria zinazotawala sekta ya usafiri wa barabarani nchini zipo chini ya mamlaka mbili tofauti huku msimamizi wa sheria zake ni Jeshi la Polisi Tanzania. Kwa upande wa Tanzania Bara sheria inayosimamia masuala ya barabarani ni Sheria ya Usalama Barabarani Sura ya 168 ya mwaka 1973 iliyorejewa mwaka 2002 na kanuni zake, na kwa upande wa Tanzania Visiwani sheria inayosimamia masuala ya barabarani ni Sheria ya Usafiri Barabarani Sura ya 7 ya mwaka 2003 na kanuni zake.

Mheshimiwa Spika, sheria zote mbili zinatambua adhabu ya tozo ya papo kwa papo kwa Tanzania Bara kifungu kinachotumika ni cha 95 Sura ya 168 ya 1973 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2002 na kanuni namba 30 ya mwaka 2015 na kwa Tanzania Visiwani kifungu kinachotumika ni cha 183 Sura ya 7 ya mwaka 2003 na kanuni namba 64 ya mwaka 2014.

Mheshimiwa Spika, katika kudhibiti makosa ya usalama barabarani ambayo yanasababisha ajali zinazoleta vifo, ulemavu, majeraha na uharibifu wa mali. Serikali kupitia Jeshi la Polisi linahimiza sheria na kanuni zilizowekwa zifuatwe kama zilivyoelezwa kwa mamlaka zote zinazosimamia usalama barabarani na usafiri wa barabarani ili kuzuia ajali barabarani zisitokee. Nakushukuru.