Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati boma la kihistoria la Mjerumani lililopo Wilayani Mkalama ili liendelee kuweka historia na kumbukumbu kwa vizazi vijavyo na kuzalisha mapato kwa Serikali?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri.

Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Mkalama ni wilaya mpya na ina mapato madogo sana. Naomba tu niseme Wizara itakuwa tayari kulipokea boma hili kama sisi Halmashauri ya Mkalama tutaamua kuwakabidhi ili walikarabati liweze kuleta manufaa kwa nchi na kwa jamii ya Mkalama; swali la kwanza. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Naibu Waziri atakuwa tayari baada ya Bunge twende naye mpaka Mkalama ili akaone hali halisi ya boma hili na aone umuhimu wake ili aharakishe mchakato wa kulichukua kama tutawakabidhi? Ahsante. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nianze kwa kumpongeza sana Mheshimiwa Francis Mtinga, amekuwa ni mfuatiliaji sana kwenye eneo hili la kuboresha malikale likiwemo hili boma la historia lililoko katika Wilaya ya Mkalama. Nimpongeze sana na pia niwapongeze wananchi wa Mkalama Iramba Mashariki kwa kuwa na Mbunge mahiri anayefuatilia maeneo haya ya kihistoria ambayo ni mojawapo ya chanzo cha mapato katika nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, nimuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kwa kuwa haya maeneo ni maeneo muhimu kwa ajili ya kuhamasisha utalii lakini pia kuongeza mapato katika sekta zetu hizi, nimuahidi kwamba tutaenda kulitembelea lakini pia kama Halmashauri itashindwa kulikarabati boma hili basi Wizara iko tayari kulipokea na kulikarabati na liwe eneo mojawapo ya chanzo cha mapato katika Serikali, ahsante. (Makofi)

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati boma la kihistoria la Mjerumani lililopo Wilayani Mkalama ili liendelee kuweka historia na kumbukumbu kwa vizazi vijavyo na kuzalisha mapato kwa Serikali?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, ahsante; Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni mtu ambaye anaheshimika Tanzania na duniani kote na kwa kufanya hivyo kule Butiama ni sehemu ambayo amezaliwa lakini pia ni sehemu ambayo amezikwa.

Je, ni kwa nini sasa Serikali haioni umuhimu wa kuboresha maeneo yale ya Hayati ili pawe ni historical site ambapo ataelezea kila kitu ili tuweze kupata watalii wengi na kuongeza mapato kama vile ilivyo kwa mwenzetu Hayati Mandela wa Afrika Kusini ambapo watu wengi wanakwenda wanamimika kuweza kujifunza zaidi? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali ina maeneo mengi ya kihistoria, lakini tuna eneo muhimu la kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere lililoko kule Butiama. Serikali ina mpango wa kuanzisha utalii wa Kiswahili, tuanita Swahili Tourism ambayo kwenye maeneo haya yenye kumbukumbu tutaanzisha Swahili Tourism iwe ni motisha; mtalii anapofika kwenye maeneo hayo basi kwanza atajifunza Kiswahili lakini atasimuliwa historia na kumbukumbu ya waasisi wetu walikuwaje na walifanya nini na ukizingatia kwamba Mwalimu Nyerere alikuwa ni mmojawapo wa waasisi wa kuboresha lugha yetu hii ya Kiswahii.

Nimhakikishie tu Mbunge kwamba eneo hili ni la muhimu na Mbunge wa eneo hilo alishanialika kwenda kule kwa ajili ya kuangalia namna ya kuboresha eneo hili ili liwe chanzo cha mapato ya Serikali. Kwa hiyo, niwatoe wasiwasi Wabunge na hata wale wengine ambao wana maeneo mengine yenye historia kupitia bajeti hii mliyotupitishia tutahakikisha kwamba maeneo haya tunayasimamia kikamilifu ili kuweza kuboresha sekta yetu hii ya utalii, ahsante. (Makofi)

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati boma la kihistoria la Mjerumani lililopo Wilayani Mkalama ili liendelee kuweka historia na kumbukumbu kwa vizazi vijavyo na kuzalisha mapato kwa Serikali?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; sera yetu ya utalii mbali ya kwamba inatuingizia mapato, pia wananchi wanaozunguka maeneo yenye hifadhi pia wananufaika. Halmashauri ya Mji wa Bunda imezungukwa na mbuga ya Serengeti.

Sasa swali langu, Mheshimiwa Waziri mbali ya kwamba wananchi wanalinda Hifadhi ya Serengeti lakini tembo wanapokuja kwa wananchi kuharibu mazao pamoja na nyumba zao wamekuwa hawalipwi fidia. Kwa mfano, Mcharo wananchi 350, Guta, 403, Bunda Store, 86, Kunzugu 65, Nyatwali 51 na Mheshimiwa Waziri nimeshaleta ofisini kwako watu hawa wanadai fidia kwa muda mrefu takriban watu 900. Lini watalipwa fidia yao? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimtoe wasiwasi Mbunge. Mbunge wa Jimbo alishawahi kunifuata akanipa orodha ya wanaodai, lakini pia hata yeye mwenyewe ameshanipa orodha ya wanaodai. Kwa hiyo, tulikubaliana kwamba nitaenda mimi mwenyewe kuongea na wananchi, lakini wale wote wanaodai nitahakikisha kwamba Serikali imewalipa, lakini pia tutaongea na wananchi waendelee kuwa wahifadhi, maana hao ndiyo wanaotusaidia sisi hata kuhifadhi maeneo yanayozunguka hifadhi, ahsante. (Makofi)