Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 507 2021-06-28

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakarabati boma la kihistoria la Mjerumani lililopo Wilayani Mkalama ili liendelee kuweka historia na kumbukumbu kwa vizazi vijavyo na kuzalisha mapato kwa Serikali?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga, Mbunge wa Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa Sera ya Malikale ya mwaka 2008, watu binafsi, Taasisi za Umma na Taasisi za Kidini, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa zinaruhusiwa kuhifadhi, kuendeleza na kunufaika na urithi wa malikale.

Mheshimiwa Spika, Sheria ya Mambo ya Kale Sura 333 kifungu cha 16 kinazipa mamlaka Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa kutunga sheria ndogo ndogo za kutunza na kuhifadhi maeneo ya malikale katika maeneo yao. Boma la kihistoria lililopo Wilaya ya Mkalama linasimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mkalama. Hivyo, tunaishauri Halmashauri husika kulikarabati na kulihifadhi ili kiwe chanzo cha mapato na Halmashauri iweze kunufaika.

Mheshimiwa Spika, Wizara iko tayari kutoa ushirikiano na miongozo ya namna ya kulikarabati na kulihifadhi boma hilo la kihistoria lililopo Mkalama ili kulindwa kwa mujibu wa Sheria ya Mambo ya Kale. Ahsante.