Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - (a) Je, kwa nini kipande cha reli ya kati kutoka Manyoni hadi Singida hakipo kwenye mpango wa ukarabati? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kukarabati kipande hicho cha reli ili kusaidia kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Singida?

Supplementary Question 1

MHE. NUSRAT SH. HANJE: Mheshimiwa Spika ahsante, pamoja na majibu Mheshimiwa Waziri, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Mkoa wa Singida ni mkoa muhimu sana pamoja na Mkoa wa Dodoma na Simiyu katika uchumi wa nchi, kwa sababu inatambulika kwamba Singida sasa hivi ni pilot kwenye zao la alizeti mahususi kwa ajili ya nchi, kwa hiyo pamoja na jibu lake kwamba mwaka 2022/2023 kwamba ndio ataweka kwenye mpango.

Je, Wizara haioni umuhimu wa kutafakari upya jambo hili kulinganisha na umuhimu wa Mkoa wa Singida kwa sasa kwenye bajeti ya mwaka huu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mkoa wa Singida kwenye miundombinu ya barabara bado kuna changamoto sana. Je, Wizara ina mpago gani wa kuhakikisha kwamba inaunganisha Mkoa wa Singida kwa barabara za lami ili kuhakikisha kwamba wakulima wa alizeti na vitunguu wanafikiwa mpaka kwenye vijiji vyao? Ahsante.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ahsante na naomba nijibu mswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge Nusrat kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza naomba nifanye marekebisho huu mwaka unasomeka 2021/2022; maana yake kuanzia Julai tathmini inafanyika tuweze kupata gharama ili tulipishe eneo la kipande cha reli ambacho kimetajwa.

Sehemu ya pili; Mheshimiwa Mbunge amesema kuunganisha barabara hizi za lami kwenye eneo lake Mkoa wake wa Singida, ni kweli kwamba tunao utaratibu mzuri wa kila Mkoa, kwa maana Meneja wa TANROADS Mkoa anapaswa kuratibu zoezi la barabara katika Mkoa wake husika. Sasa tupokee hoja yako kama kuna eneo ambalo halipitiki kabisa kwa sasa, nielekeze Meneja wa TANROADS wa Mkoa wa Singida afanyie kazi kama kuna sehemu ya kuchukua dharura tufanye hivyo ili kufanya maboresho kwa wakulima wa alizeti, vitunguu na maeneo mengine wapate huduma nzuri ya usafiri, ahsante.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: - (a) Je, kwa nini kipande cha reli ya kati kutoka Manyoni hadi Singida hakipo kwenye mpango wa ukarabati? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kukarabati kipande hicho cha reli ili kusaidia kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Singida?

Supplementary Question 2

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Spika, nakushkuru sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ni miundombuni ya reli ni muhimu sana katika usafirishaji wa mizigo pamoja na abiria, na kwa sababu reli hii ilianzishwa na Baba wa Taifa; Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kumuenzi Baba wa Taifa kwa kuifanyia haraka kuijenga reli hii na iweze kutumika?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA): Mheshimiwa Spika, ninaomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mtaturu, Mbunge kutoka Mkoa wa Singida kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi kwamba Serikali inatambua umuhimu wa reli hii, kama alivyosema imeasisiwa na Baba wa Taifa, na tukifanya tathmini ya kujua gharama tutaiboresha reli hii. Hii reli iliopo ni ya zamani itabadilishwa tuweke iwe kubwa zaidi iweze kubeba mzigo mkubwa zaidi.

Kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge tupe muda mwaka huu mpaka mwakani utapata majibu ya ujenzi wa reli Singida
– Manyoni na maeneo mengine.