Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 504 2021-06-28

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NUSRAT S. HANJE aliuliza: -

(a) Je, kwa nini kipande cha reli ya kati kutoka Manyoni hadi Singida hakipo kwenye mpango wa ukarabati?

(b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kukarabati kipande hicho cha reli ili kusaidia kuchochea ukuaji wa uchumi wa mkoa wa Singida?

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. MWITA M. WAITARA) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Shaaban Hanje, Mbunge wa Viti Maalum lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kupitia Shirika la Reli Tanzania (TRC) inaendelea na mpango wa ukarabati wa mtandao wa reli iliyopo na kufufua njia za reli zilizofungwa kwa awamu kwa kuanzia na njia kuu (main line). Katika kutekeleza jukumu hilo, Serikali inazingatia Mpango wa Miaka Mitano wa Taifa ambao unaanzia 2021/ 2022 – 2025/2026. Aidha, Serikali itaendelea na ukarabati wa matawi ya reli ikiwemo kipande cha reli kutoka Manyoni hadi Singida kulingana na mahitaji ya ukuajiwa uchumi na uwezo wa kifedha. Lengo la Serikali ni kuboresha miundombinu ya reli ili kurahisisha huduma za uchukuzi nchini.

Mheshimiwa Spika, sehemu (b); Serikali inatambua umuhimu wa kuwepo na miundombinu ya reli imara katika kuchochea uchumi wa nchi. Hata hivyo, kama nilivyoeleza katika jibu langu la msingi sehemu (a), Serikali itaendelea kufungua njia zote zilizokuwa zimefungwa ikiwa ni mkakati wake wa kurejesha huduma za usafiri wa reli wenye uhakika nchini na kuchochea ukuaji wa uchumi.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali kupitia TRC imepanga kufanya tathmini kwa ajili ya ufunguaji wa njia zilizokuwa zimefungwa kwa lengo la kujua gharama za ukarabati. Maeneo ya reli yatakayohusika ni pamoja na Kilosa – Kidatu na Manyoni – Singida. Hivyo, naomba Mheshimiwa Mbunge aelewe kwamba Serikali inafanya kazi eneo la reli Manyoni – Singida, ahsante.