Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusafisha na kuongeza kina cha Bwawa la Maji Lukuledi-Masasi linalohudumia Vijiji vya Lukuledi, Nambawala, Mraushi, Mwangawaleo na Ndomoni?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwanza nashukuru kwa majibu mazuri yenye matumaini yaliyotolewa na Mheshimiwa Waziri kwa wananchi wa maeneo ambayo walikuwa na shida kubwa ya maji, lakini pamoja ma majibu hayo mazuri naomba kuuliza Mheshimiwa Waziri kwamba kwa kuwa katika Kata za Mpanyani, Namatutwe, Msikisi, Namajani ambao pia Nambawala ipo katika Kata ya Mpanyani, wananchi hawa hawajawahi kuona maji salama kwa maana ya mabomba na naomba kuuliza; je, Serikali ina mpanga gani wa kuharakisha uchimbaji wa mabwawa katika kata hizo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika Kijiji cha Mraushi na vitongoji vyake ambapo katika majibu ya msingi Serikali imethibitisha kwamba ujenzi wa mradi wa kuwapatia maji wananchi hao umeanza kwa bajeti ya mwaka 2021/2022. Ni lini mradi huo utakamilika ambapo pia nina uhakika Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kuambatana na mimi kwenda kujionea kadhia ya hali ya maji katika maeneo hayo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza nimpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji wake mkubwa na si mara moja amekuja katika Wizara yetu ya Maji kuhakikisha wananchi wake kuwa wanapata huduma ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, kwanza nilishukuru sana Bunge lako Tukufu sisi Wizara ya Maji kutuidhinishia zaidi ya shilingi bilioni 680. Lakini kwa namna ya kipekee Mheshimiwa Rais kwa dhamira yake njema ya kuhakikisha kwamba anakwenda kumtua mwana mama ndoo kichwani ametupatia fedha ya nyongeza zaidi ya shilingi bilioni 207; haijawahi kutokea; nataka nimuhakikishie fedha zile moja ya mipango ni kuhakikisha kwamba tunakwenda kununua vitendea kazi kwa maana ya magari ya kisasa kwa ajili ya ujengaji wa mabwawa pamoja na uchimbaji wa visima. Kata zake alizoainisha tutakwenda kuzipa kipaumbele katika kuhakikisha kwamba tunakwenda kutatua tatizo la maji. Ahsante sana.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kusafisha na kuongeza kina cha Bwawa la Maji Lukuledi-Masasi linalohudumia Vijiji vya Lukuledi, Nambawala, Mraushi, Mwangawaleo na Ndomoni?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwenye Wilaya ya Kyerwa kuna mradi wa vijiji 57, mradi huu Serikali imesema utajengwa kwa awamu, lakini kwenye bajeti kuna Kata ya Kikukulu, Kata ya Songembele, Kichwechwemkula na Rukaija havikuwekwa bajeti. Nini kauli ya Serikali juu ya kata hizi ambazo hazikuwekwa kwenye bajeti? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kaka yangu Bilakwate kwa namna anavyopigania jimbo lake la Kyerwa, kubwa ambalo nataka nimuhakikishie mkakati wa Wizara yetu ya Maji ni kuhakikisha tunatumia vyanzo toshelevu ikiwemo Mto Kagera.

Sasa moja ya vijiji ambavyo vingi tunakwenda kutatua tatizo la maji zaidi ya 50. Tumesema mradi huu tunakwenda kuutekeleza kwa awamu, kata ambazo hazipo katika bajeti hii tutahakikisha bajeti ijayo tunaziweka ili kuhakikisha kwamba wananchi wake wanaweza kupata huduma hii muhimu ya maji. Ahsante sana.