Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 60 Water and Irrigation Wizara ya Maji 501 2021-06-28

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kusafisha na kuongeza kina cha Bwawa la Maji Lukuledi-Masasi linalohudumia Vijiji vya Lukuledi, Nambawala, Mraushi, Mwangawaleo na Ndomoni?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha maeneo mbalimbali yanapata huduma ya maji ya uhakika na kipaumbele ni maji kwa matumizi ya nyumbani ambapo Vijiji vya Lukuledi, Ndomoni na Nambawala vinapata huduma ya maji safi, salama na yenye kutosheleza.

Katika mwaka wa fedha 2021/2022 kazi ya ujenzi wa miundombinu ya kufikisha maji Kijiji cha Mraushi pamoja na Kitongoji cha Mwangawaleo, utekelezaji unaendelea ambapo utahusisha ulazaji wa bomba lenye urefu wa kilometa sita, vituo vya kuchotea maji 16 na ujenzi wa tanki la lita 100,000 kuongeza upatikanaji wa maji katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Vijiji vya Lukuledi, Nambawala, Mraushi na Ndomoni wanatumia maji ya Bwawa la Lukuledi. Hivyo, kutokana na umuhimu huo katika mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali itakamilisha usanifu na kuanza ukarabati wa bwawa hilo ili liwe na uwezo wa kuhifadhi maji mengi ya kukidhi mahitaji ya shughuli hizo za maendeleo.