Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika vijiji 14 vya Jimbo la Manyoni Magharibi?

Supplementary Question 1

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa nafasi; pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa Kata za Rungwa, Ipande na Kitaraka za Jimbo la Manyoni Magharibi hazina umeme kabisa jambo ambalo linakwamisha jitihada za wanawake na vijana kujikomboa kiuchumi.

Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kupeleka umeme katika umeme vijiji hivyo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa vijiji vya Kinyamwenda, Itaja na Ngimu vya Jimbo la Singida Kaskazini ambavyo vilikuwa katika mpango wa mradi wa backbone unaoanzia Singida, Arusha hadi Namanga havina umeme kabisa.

Je Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha vijiji hivi vinakuwa na umeme? Nakushukuru.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Aysharose Mattembe kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kuwa amekuwa mstari mbele sana kufuatilia upelekaji wa umeme katika Mkoa wote wa Singida na tumekuwa mara kwa mara tukijadiliana na kuhakikishia kwamba hakika tutafikisha umeme katika maeneo yote ya Kinyamwenda kama alivyosema, Kitalaka na kata nyingine ambazo ziko katika maeneo yake.

Mheshimiwa Spika, kama tulivyosema mkandarasi anayetarajiwa kupeleka umeme katika Mkoa wetu wa Singida kwenye Wilaya yetu ya Manyoni ataanza kazi mwezi unaokuja na tutahakikisha kwamba vijiji hivyo vyote 14 ambavyo vilikuwa vimebakia bila kupelekewa umeme vinapata umeme.

Mheshimiwa Spika, lakini katika swali la pili hayo maeneo mengine ambaye ameyasema yamechukuliwa na mkandarasi ambaye anapeleka umeme kutoka Iringa kupita Dodoma, Singida kwenda Arusha kwenda mpaka Namanga na viko katika scope yake na kazi yake inatakiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi wa saba.

Mheshimiwa Spika, tunafahamu kwamba tayari vifaa vya kufanya kazi hiyo vipo site kwa maana ya nguzo, waya na transfoma na tutahakikisha kwamba tunasimama naye ili katika muda aliopewa aweze kukamilisha kazi hiyo ili wananchi wote wa Singida waweze kupata umeme kwa ajili ya maendeleo katika maeneo yao, ahsante.

Name

Kwagilwa Reuben Nhamanilo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Handeni Mjini

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika vijiji 14 vya Jimbo la Manyoni Magharibi?

Supplementary Question 2

MHE. KWAGILWA R. NHAMANILO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kuuliza swali moja la nyongeza; ni lini Serikali itapeleka umeme kwa vijiji 28 ambavyo viko katika Jimbo la Handeni Mjini havijapata umeme mpaka sasa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kwagilwa Mbunge wa Handeni Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimshukuru pia na yeye kwa kuendelea kufuatilia upelekaji wa umeme katika maeneo yake. Jimbo la Handeni Mjini halina tofauti na Jimbo la Bukoba Mjini ambao ni maeneo ambayo hayakuwa yananufaika na Mradi wa REA, lakini sisi tumeweka katika mradi wa peri urban ambao tunatarajia kuuanza mwezi wa tisa na hivyo maeneo yote ya mijini ambayo pengine bado yanaonekana yana nature ya vijiji; Jimbo la Bukoba Mjini, Handeni Mjini na maeneo mengine yakiwepo yatapelekewa umeme kuanzia mwezi wa tisa kupitia mradi wetu wa peri urban ikiwa ni pamoja na Ilemela, Mwanza na maeneo kama ya Geita ambayo yako mjini, lakini yana hadhi ambayo ya kijijini. Nashukuru.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika vijiji 14 vya Jimbo la Manyoni Magharibi?

Supplementary Question 3

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana; kwanza nikupongeze wewe kwa kazi nzuri ambayo unaifanya kuelekea kuhitimisha Bunge letu la Bajeti.

Mheshimiwa Spika, naomba niulize swali la nyongeza, lakini kabla ya kuuliza kwanza niipongeze Serikali na Wizara ya Nishati kwa kazi nzuri na kubwa inayoifanya kwa sababu wakati Wizara ya Nishati inatoa taarifa yake ilisema itamalizia umeme REA Awamu ya Tatu vijiji vyote vya Tanzania.

Mheshimiwa Spika, na ninataka niwahakikishie kwamba katika Jimbo langu la Mchinga wataalam wako kazini tangu tarehe 16 mwezi huu wa Juni wakiwa na mkandarasi anayeitwa Nakuroi Investment Company Limited wanafanya kazi nzuri sana. Vijiji vyote kama Kijiji cha Kiwawa, Mputwa, Ruvu na Mtamba, Luchemi, Lihimilo Mnyangala, Namkongo, Makangala na Luhoma; hivi vijiji vyote vimeshafikiwa, isipokuwa kuna vijiji viwili tu ambavyo vimesahaulika. (Makofi)

Nakuomba sana na ninaiomba Serikali katika awamu ile ya tatu wamalizie hivyo vijiji viwili ambavyo ni Kijiji cha Dimba na Kijiji cha Kitohave. Ahsante sana Mheshimiwa Waziri.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nipende kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete, Mbunge wa Mchinga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nianze kwa shukrani kwa niaba ya Wizara, lakini na Serikali kwa Mheshimiwa Mbunge kuona kwamba Serikali kwa ujumla yake chini ya uongozi wa Mheshimiwa wa Mama Samia Suluhu Hassan imeamua kuhakikisha kwamba inawafikishia umeme Watanzania wote mahala walipo, na kupitia mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili kuhakikisha vijiji vyote ambavyo amekuwa amepelekewa umeme vinapelekewa.

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Wabunge wengine tunafurahi kwamba sasa wakandarasi katika maeneo yetu mengi tayari wako site, kazi tayari zimeanza za kufanya survey na kuhakiki vijiji ambavyo vimechukuliwa na vitapewa umeme.

Mheshimiwa Spika, niwaombe Waheshimiwa Wabunge wale ambao katika maeneo yao hawajawaona wakandarasi au wameendelea kupata changamoto ya mawasiliano na wakandarasi hao basi tuwasiliane ili tuweze kuhakikisha kwamba tunasimamiana ili katika muda ambao tumewahakikishia Waheshimiwa Wabunge kwamba tutapeleka umeme katika maeneo yetu, tuweze kufikisha umeme kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, juzi Mheshimiwa Waziri alisema kwamba vilikuwa vimebaki vijiji kama 680 ambavyo havikuwa vimeingia kwenye ile awamu yetu, lakini tayari maelekezo yametolewa na vijiji vyote vilivyoko katika maeneo yetu vimechukuliwa na vitafanyiwa kazi katika Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili bila kuacha hata kijiji kimoja.

Mheshimiwa Spika, hii ni commitment ya Serikali kwamba ifikapo Disemba, 2022 vijiji vyote ambavyo viko katika maeneo yetu vitakuwa vimepata umeme na kuhakikisha kwamba wananchi wote wanaendelea kufarijika na huduma ya umeme kwa ajili ya maendeleo katika maeneo yetu nashukuru sana.