Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 59 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 495 2021-06-25

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AYSHAROSE N. MATTEMBE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka umeme katika vijiji 14 vya Jimbo la Manyoni Magharibi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Aysharose Ndogholi Mattembe, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kazi ya kupeleka umeme katika vijiji 14 pamoja na vijiji vingine vilivyobaki katika Jimbo la Manyoni Magharibi itaanza mwezi Julai, 2021 kupitia utekelezaji wa mradi wa REA Awamu ya Tatu Mzunguko wa Pili. Mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Disemba, 2022.

Mheshimiwa Spika, kazi ya utekelezaji wa mradi huu katika Wilaya ya Manyoni kwa ujumla inahusisha ujenzi wa njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 33 urefu wa kilometa 383.1, njia ya umeme ya msongo wa kilovoti 0.4 urefu kilometa 31, ufungaji wa transfoma 31 zenye uwezo wa KVA 50 pamoja na kuunganisha huduma ya umeme kwa wateja wa awali 682. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 15.45.