Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Nassor Amar

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyang'hwale

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Magu –Ng’hungumalwa kwa kiwango cha lami utaanza baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN N. AMAR: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Serikali ilishapitisha ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Geita kwenda Nyang’hwale, tulikuwa tukipewa kilomita nne kila mwaka na sasa hivi tumeshajengewa zaidi ya kilomita nane; miaka miwili iliyopita hatujapewa tena hizo kilomita nne nne: -

Je, Serikali inatoa kauli gani; imeifuta hiyo barabara kwa ujenzi wa lami au la?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, alivyosema Mheshimiwa Hussein Amar Mbunge barabara ya Geita hadi Nyang’hwale ni barabara ambayo tayari imeshaanza kujengwa na Serikali haijaifuta barabara hiyo kuijenga kwa kiwango cha lami. Tumhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba barabara hii itaendelea kujengwa kadri fedha itakavyoendelea kupatikana. Kwa hiyo, haijaifuta na haina mpango wa kuifuta, lakini itategemea na upatikanaji wa fedha hili kuendeleza ujenzi wa barabara hiyo kwa kiwango cha lami. Ahsante. (Makofi)

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Magu –Ng’hungumalwa kwa kiwango cha lami utaanza baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa viongozi wakuu waliahidi kiwango cha kilimeta 10 katika Mji wa Karatu mwaka 2010 – 2015 na 2015 - 2020 mpaka leo hii hatuna hata kilometa moja: sasa ni lini ahadi ya viongozi wakuu itatekelezwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, kama alivyosema Mheshimiwa Awack kuhusu ahadi za Viongozi wa Kitaifa ya kujenga barabara kilometa kumi katika Mji wa Babati, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kazi ya Serikali ni kujenga barabara hizo kama zilivyoahidiwa na Viongozi wa Kitaifa. Ujenzi huo kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi zitajengwa katika awamu hii ya miaka mitano. Kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge avute subira na kadri bajeti itakavyoruhusu, hiyo barabara ya kilomita 10 itajengwa katika Mji wa Babati. Ahsante.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Magu –Ng’hungumalwa kwa kiwango cha lami utaanza baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 3

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Serikali imejiridhisha kuwa barabara ya kuanzia Dochi kupitia Ngulwi hadi Mombo ambayo ni kilometa 16 kuwa itajengwa na TANROADS: -

Je, ni lini barabara hiyo itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kama alivyosema Mheshimiwa Shekilindi barabara ya Dochi - Mombo yenye urefu wa kilomita 16 itajengwa na TANROAD, lakini katika mpango huu kwa mwaka huu wa bajeti, barabara hii haimo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba TANROADS kupitia Serikali, barabara hii katika mipango ijayo itajengwa kama ilivyoahidiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: - Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Magu –Ng’hungumalwa kwa kiwango cha lami utaanza baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?

Supplementary Question 4

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Murushaka kwenda mpaka Mrongo ni barabara ya kiuchumi kwa Mkoa wa Kagera, lakini pia ni barabara muhimu inayounganisha nchi ya Tanzania na Uganda; na kwa umuhimu wake Mheshimiwa Hayati Pombe Magufuli aliahidi ijengwe kilometa 50 za haraka. Ni lini kilometa 50 hizi zitajengwa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli barabara ya Mrongo yenye urefu wa kilomita 112 aliyoitaja Mheshimiwa Bilakwate ni kweli iliahidiwa na Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Naibu Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, barabara hii imeingizwa kwenye mpango na fedha imetengwa kwa ajili ya kuanza mwaka wa fedha ujao kwa kiwango cha lami. Nadhani tumetenga kama siyo chini ya shilingi bilioni tatu kwa kuanzia. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa wa Kyerwa na wananchi wa Kyerwa, ahadi ya Mheshimiwa Rais Hayati itaanza kutelekezwa mara tutakapoanza utekelezaji wa bajeti ambayo Bunge lako imelipitisha. Ahsante.