Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 58 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 489 2021-06-24

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA aliuliza: -

Je, ni lini ujenzi wa barabara ya Magu –Ng’hungumalwa kwa kiwango cha lami utaanza baada ya upembuzi yakinifu kukamilika?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Boniventura Destery Kiswaga, Mbunge wa Magu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Kazi ya upembuzi yakinifu na usanifu wa kina kwa ajili ya ujenzi wa kiwango cha lami, barabara ya Magu – Bukwimba - Ngudu – Ng’hungumalwa yenye urefu wa kilometa 71 ilikamilika mwaka 2019.

Katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali imetenga shilingi milioni 1,500 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kilometa 10 kwa kiwango cha lami barabara hii. Serikali itaendelea na ujenzi wa barabara hii kadri ya upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.