Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:- Moja kati ya vikwazo vya utekelezaji wa Ilani ya CCM ni kutotolewa kwa fedha kwa ukamilifu na kwa wakati:- (a) Je, ni kiasi gani cha fedha kilikasimiwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa mwaka wa fedha 2015/2016? (b) Je, Serikali imetoa kiasi gani cha fedha za Miradi ya Maendeleo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Msalala hadi kufikia Desemba, 2015? (c) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha fedha za maendeleo zinapatikana kwa wakati na kupelekwa kwenye miradi husika?

Supplementary Question 1

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri, kumekuwana kisingizio kikubwa cha sababu ya ucheleweshaji wa fedha kwa kutokukamilika kwa miradi mingi na kupelekea wakandarasi kudai kwamba wanalipwa kidogo kidogo. Kwa mfano, miradi ya maji ambayo iko katika Kijiji cha Ipalamwa, Kitoho, Ilamba na sehemu nyingine. Sasa Serikali inasemaje, nani wa kuchukuliwa hatua, ni Halmashauri husika au Mkandarasi ambaye ameshindwa kumaliza mradi kwa wakati na ubora?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, fedha zinapelekwa kulingana na certificate ambayo mkandarasi ameiwasilisha Halmashauri na imefanyiwa tathmini na imewasilishwa Wizara ya Maji ndiyo tunapeleka fedha kulingana na kiwango cha uzalishaji ambacho Mkandarasi amezalisha. Kwa hiyo hapo, Wakurugenzi wanaagizwa kuwasukuma wakandarasi waweze kuzalisha zaidi ili Serikali iweze kutoa fedha zaidi.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:- Moja kati ya vikwazo vya utekelezaji wa Ilani ya CCM ni kutotolewa kwa fedha kwa ukamilifu na kwa wakati:- (a) Je, ni kiasi gani cha fedha kilikasimiwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa mwaka wa fedha 2015/2016? (b) Je, Serikali imetoa kiasi gani cha fedha za Miradi ya Maendeleo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Msalala hadi kufikia Desemba, 2015? (c) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha fedha za maendeleo zinapatikana kwa wakati na kupelekwa kwenye miradi husika?

Supplementary Question 2

MHE. KANGI A. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ucheleweshaji wa fedha kwenye miradi ya maendeleo limejitokeza kwenye Jimbo la Mwibara ambako Miradi ya Maji ya Bulamba, Kibara pamoja na maji ya Mji wa Bunda kutoka Nyabehu, zaidi sasa ya miaka saba, fedha bado zinacheleweshwa kwenda. Hili ambalo analisema Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, lazima certificate zile ziandaliwe na zihakikiwe, sisi Halmashauri ya Wilaya ya Bunda kwa kushirikiana na Engineer ya Maji wa Wilaya, tulishasukuma sana hizi certificate na kuna mabarua mengi Wizara ya maji. Sasa je, Mheshimiwa Naibu Waziri ataliambia vipi Bunge hili kwamba hata zile certificate ambazo zilishahakikiwa bado fedha haziendi, ni uzembe wa Wizara au ni uzembe wa mtu gani? Ahsante.

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge tuwasiliane moja kwa moja, aje ofisini kwa sababu sina taarifa kwamba kuna certificate ambayo haijalipwa. Juzi Mheshimiwa Waziri wa Fedha ametoa bilioni 15 na certificate zote zimelipwa, sina pending certificate ambayo imebaki kwenye ofisi ambayo haijalipwa. Kwa hiyo, kurahisisha kazi Mheshimiwa Mbunge, naomba awasiliane na mimi ili tuweze kuangalia ni nini kimetokea.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:- Moja kati ya vikwazo vya utekelezaji wa Ilani ya CCM ni kutotolewa kwa fedha kwa ukamilifu na kwa wakati:- (a) Je, ni kiasi gani cha fedha kilikasimiwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa mwaka wa fedha 2015/2016? (b) Je, Serikali imetoa kiasi gani cha fedha za Miradi ya Maendeleo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Msalala hadi kufikia Desemba, 2015? (c) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha fedha za maendeleo zinapatikana kwa wakati na kupelekwa kwenye miradi husika?

Supplementary Question 3

MHE. SUBIRA K. MGALU: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, ninayo maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kwa mujibu wa jibu lake la msingi Mheshimiwa Naibu Waziri, ameonesha kuna bakaa ya fedha ambazo zimebaki hazijawasilishwa kwenye Halmshauri ya Wilaya ya Msalala, kiasi kwamba itapelekea miradi kutokamilika kwa wakati. Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, anaweza kulihakikishia Bunge hili kabla ya mwaka wa fedha mpya haujaanza miradi ile itakamilika na Serikali itapeleka fedha?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa swali la msingi limeelekeza changamoto ya upelekaji wa fedha za maendeleo ambalo ni changamoto inayoikabili karibu nchi nzima kwa mwaka huu wa fedha, hususani, Halmashauri zetu za Mkoa wa Pwani. Je, Naibu Waziri yupo tayari kutoa maelekezo kwa Wakurugenzi kwa miradi ambayo ni viporo hasa ya Sekta ya Afya, wawasilishe taarifa haraka ili Serikali iweze kuikalimisha katika Halmashauri mbalimbali za Mkoa wa Pwani?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, bajeti pale mpaka mwezi Desemba, nimesema zilikuwa hazijafikia shilingi bilioni 3.1 zilizokuwa zimepelekwa, lakini mpaka mwezi Mei, hivi sasa fedha ambazo zimepelekwa katika ile bajeti imefika bilioni mbili (2), lakini fedha zingine za nje zimeongezeka na zimefikia karibu bilioni 1.9 mwezi uliopita. Kwa hiyo, jukumu kubwa ni nini? Tunaona kwamba kuanzia mwezi Desemba, mpaka hivi sasa kuna fedha nyingine za Serikali zimezidi kupelekwa na hapa maana yake Serikali itajitahidi kwa kadiri iwezekanavyo ili miradi iliyokusudiwa iweze kukamilika.
Mheshimiwa Naibu Spika, isipokuwa katika hili, ni lazima wataalam wetu, wakati mwingine ule uwezo wa utumiaji wa fedha za miradi kwa watendaji wetu umekuwa ni udhaifu zaidi. Kwa mfano, hapa tunapozungumza fedha nyingi zimeshapelekwa kule Msalala, basi nawaomba watendaji wetu waweze kuhakikisha kwamba, fedha zilizofika za maendeleo zitumike ilimradi wananchi waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni jinsi gani tutafanya kwa Mkoa wa Pwani. Kikubwa zaidi naomba niwaagize kama nilivyosema, ni kwamba Wakurugenzi wote wa Mkoa wa Pwani na mikoa mingine yote katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wahakikishe kwambam kwanza wanaandaa zile changamoto zilizokuwepo katika Sekta ya Afya na miradi mingine, lakini tubainishe kwamba hata hizo fedha zilizofika ziweze kutumika kwa ajili ya maslahi ya wananchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika hili, naomba nitoe onyo kwa Wakurugenzi mbalimbali, kipindi cha mwaka unapofika siku hizi za mwisho, watu wamekuwa wakifanya mambo ya ajabu sana katika matumizi ya fedha za Serikali, wakijua kwamba mwaka unakwisha. Wakati mwingine fedha zinapelekwa sehemu ambazo hata zisizohusika, ambazo haziendi kuwagusa wananchi. Kwa mwaka huu naomba nikiri wazi kwamba, Mkurugenzi yeyote ambaye atacheza na fedha za Serikali, naamini Waziri wangu ataamua kuchukua fimbo kubwa sana kuhakikisha kwamba watu hawa wanawajibishwa. Lengo kubwa kuhakikisha wananchi wetu wanapata huduma kutokana na kazi kubwa inayofanywa na Serikali yao ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.