Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 445 2016-06-28

Name

Ezekiel Magolyo Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. SUBIRA K. MGALU (K.n.y. MHE. EZEKIEL M. MAIGE) aliuliza:-
Moja kati ya vikwazo vya utekelezaji wa Ilani ya CCM ni kutotolewa kwa fedha kwa ukamilifu na kwa wakati:-
(a) Je, ni kiasi gani cha fedha kilikasimiwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kwa mwaka wa fedha 2015/2016?
(b) Je, Serikali imetoa kiasi gani cha fedha za Miradi ya Maendeleo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Msalala hadi kufikia Desemba, 2015?
(c) Je, Serikali ina mikakati gani ya kuhakikisha fedha za maendeleo zinapatikana kwa wakati na kupelekwa kwenye miradi husika?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ezekiel Magolyo Maige, Mbunge wa Masalala, lenye sehemu (a), (b) na (c), kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, katika mwaka wa fedha 2015/2016, kiasi cha shilingi bilioni 4.1 kilitengwa kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, hadi kufikia mwezi Desemba, 2015 Serikali imeshatoa kiasi cha shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Msalala. Aidha, wahisani wametoa jumla ya shilingi bilioni 1.6 nje ya fedha zilizoidhinishwa katika bajeti ya Halmashauri hiyo kwa ajili ya miradi ya TASAF, SEDP na AGPHAI na kufanya fedha zote zilizopokelewa hadi Desemba, 2015 kufikia bilioni 3.1.
(c) Mheshimiwa Naibu Spika, fedha za miradi ya maendeleo zinapelekwa katika Halmashauri zote kulingana na makusanyo yanayofanyika. Mkakati uliowekwa na Serikali ni kuimarisha makusanyo ya mapato ya Serikali na kudhibiti upotevu wa mapato katika vyanzo mbalimbali ili kuhakikisha fedha zinapelekwa kama zilivyopangwa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi katika mwaka wa fedha 2016/2017.