Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. DANIEL A. TLEMAI aliuliza: - Je, Serikali ina mkakati gani wa kuendeleza mashamba ya Karatu –Bendhu pamoja na kuwalipa wafanyakazi wa mashamba hayo?

Supplementary Question 1

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu ilituma Wizarani mara nyingi kwamba kuna mashamba hayo aliyoyataja Mheshimiwa Naibu Waziri, kati ya mashamba 33 yanayoendelezwa kwa robo moja tu katika mashamba yale yote 33; lakini kwa kuwa shamba hili la Bendhu mmiliki wake alifariki na akamwachia mwanae ambayo yupo nchini Zimbabwe na baadaye wafanyakazi wale hawajaweza kulipwa muda wote tokea mmiliki yule aliyefariki namba moja na yule aliyeachiwa shamba hilo hajaweza kuonekana mpaka muda huu. Sasa ni lini majibu ya Serikali kwamba hili shamba la Bendhu wafanyakazi wale wote wanaweza kupata haki yao? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ni lini Waziri atakubaliana nami kwenda katika Jimbo la Karatu kuona mashamba haya 33 yote, ajionee kwamba haya mashamba hayaendelezwi. Kwa mfano katika Kata ya Oldeani hata mahali pa kuzika mtu hakuna kwa sababu mashamba yale yote yapo chini ya uwekezaji na wakati huo kutoka Fireland Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro imekuwa msitu mwingine baada ya Fireland ya Hifadhi ya Mamlaka ya Ngorongoro. Je, ni lini Waziri atafuatana na mimi kwenda katika Jimbo la Karatu kujionea mashamba haya hayaendelezwi katika majibu aliyotoa kwamba anaona mashamba haya yanaendelezwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Daniel, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kwenda karatu mimi na yeye tumeshakuwa na maongezi tutakwenda na tutapanga tarehe pamoja ambayo tutakwenda kutembelea, kwenda kuangalia hayo mashamba na matatizo ya wakulima wa vitunguu ambao wanakabiliana nayo. Pia kuhusu Shamba la Bendhu nimeshajibu kwenye swali la msingi Serikali sasa hivi hatuwezi kusema jambo lolote kwasababu jambo hili lipo mahakamani tunasubiri shauri hili liishe mahakamani then tunaweza kufanya intervention.