Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Mwakijembe ambao mashamba yao yalitwaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) watalipwa fidia?

Supplementary Question 1

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kata ya Mwakijembe tuna changamoto kubwa sana ya ukame. Kwa hiyo, eneo hili lililotwaliwa ndilo eneo pekee linalofaa kwa kilimo; na kwa sababu, wananchi hawa wameondolewa kwenye eneo lile.Je, Serikali iko tayari kufanya mchakato wa haraka wa kuwafidia watu hawa ili waondokane na madhila wanayoyapata sasa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili. Kwa kuwa imebainika wazi kwamba eneo hili ni hatarishi; kwa miaka miwili mfululizo yametokea mafuriko makubwa na tumewahatarisha Askari wetu kwenye eneo lile: Je, Serikali ipo tayari kuwahamisha Askari hawa kwenda kwenye eneo la awali ambalo Kamati ya Bunge ililiona ili Askari hawa wakae kwenye eneo ambalo ni salama? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kitandula, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu kwamba, ni dhamira ya Serikali kupitia Wizara yangu kuwalipa fidia wananchi wa maeneo yote ambayo yametwaliwa kwa ajili ya matumizi ya shughuli za kiulinzi. Kwa hiyo, Mheshimiwa Kitandula kama tulivyowahi pia kuzungumza, ni kwamba tunashirikiana na wenzetu Wizara ya Ardhi na Wizara ya Fedha, na yako maeneo mengi ambayo tayari tumeshalipa fidia; pia uko mpango wa Serikali kupitia Wizara ya Fedha kutupatia fedha na taratibu zikikamilika wananchi hawa nawahakikishia kwamba watalipwa mara moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, kuona umuhimu wa eneo hili kutumika tena kwa wananchi, niseme tu kwamba, labda kutokana na changamoto za mvua nyingi tulizozipata hivi karibuni, umevutiwa pia kuona uko umuhimu wa wananchi kuendelea kufanya umwagiliaji katika eneo hili; niseme tu kwamba zile sababu za kupewa eneo hili bado zipo. Hata hivyo tunaweza tukalitazama kutokana na maoni ya Mheshimiwa Mbunge kwa sababu, iko kamati maalum ambayo inaendelea kuyapitia maeneo yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie Mheshimiwa Mbune kwamba, naelekeza wafanye pia marejeo katika eneo hili kwa kushirikiana na Kamati yetu ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya na pia kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge ili tuone kama pia tunaweza tuka-reallocate, tukapata eneo lingine bila kuondoa sababu muhimu za kufanya vijana wetu waendelee kufanya shughuli zao muhimu katika eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tu kwamba tutaendelea kushirikiana ili kuona tunaweza kutenda vema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili, kuona umuhimu wa eneo hili kutumiwa tena na wananchi, labda kutokana na changamoto ya mvua nyingi tulizozipata hivi karibuni, Mbunge amevutiwa kuona kwamba upo umuhimu wa wananchi kuendelea kufanya umwagiliaji katika eneo hili. Niseme tu kwamba, zile sababu za kupewa eneo hili bado zipo, lakini tunaweza tukalitazama kutokana na maoni ya Mbunge kwa sababu ipo Kamati Maalum ambayo inaendelea kuyapitia maeneo yote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivyo, nimhakikishie tu Mbunge kwamba naelekeza wafanye pia marejeo katika eneo hili kwa kushirikiana na Kamati yetu ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya lakini kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge ili tuone kama tunaweza tuka-reallocate, tukapata eneo lingine bila kuondosha sababu muhimu za kufanya vijana wetu waendelee kufanya shughuli zao muhimu katika eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge tu kwamba tutaendelea kushirikiana ili kuona tunaweza kutenda vema.

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: - Je, ni lini wananchi wa Kata ya Mwakijembe ambao mashamba yao yalitwaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) watalipwa fidia?

Supplementary Question 2

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami niunge katika swali alilouliza ndugu yangu Mheshimiwa Dunstan Kitandula, kwamba kumekuwa na utaratibu au zoezi ambalo linaendelea kule Msata katika maeneo ya Kihangaiko na Pongwe Msungura wakipima maeneo ya wananchi katika maana ya kulipa fidia, lakini kwa taarifa nilizozipata za juzi ni kwamba zoezi lile limesimama kwa sababu ya Mkataba ambao walikuwa wamepeana baina ya Wizara na yule mpima kuhusiana na eneo lile. (Makofi)

Mheshimimiwa Mwenyekiti, sasa katika spirit ya kuondoa migogoro iliyoko baina ya Jeshi na wananchi…

MWENYEKITI: Sasa uliza swali.

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inasemaje? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ridhiwani Kikwete, maarufu kama Baba Aziza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhamira yetu kupima maeneo yote yanayomilikiwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania. Kwa hiyo huo ni utaratibu unaoendelea na nimhakikishie tu Mheshimiwa Ridhiwani, sio kwamba zoezi limesitishwa, zoezi la upimaji maeneo yote linaendelea lina hatua zake. Kwa hiyo niwatoe wasiwasi tu wananchi wa eneo la Msata Kihangaiko, wanavyoona wale wapimaji hawapo wanafikiri labda shughuli imesita, hapana.

Nimtoe wasiwasi pia Mheshimiwa Ridhiwani zoezi linaendelea, tutahakikisha maeneo yote tunamaliza kufanya upimaji na wananchi wanapata haki zao. (Makofi)