Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 57 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 481 2021-06-23

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA aliuliza: -

Je, ni lini wananchi wa Kata ya Mwakijembe ambao mashamba yao yalitwaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) watalipwa fidia?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dunstan Luka Kitandula, Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lilianzisha Kituo cha Ulinzi mwaka 2017, eneo la Kata ya Mwakijembe. Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Mkinga Mkoani Tanga iliona umuhimu wa kutenga eneo hilo kwa matumizi ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania ili kuimarisha ulinzi kwenye maeneo ya mpakani. Aidha, Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama ilitembelea eneo husika mwaka 2017 kujionea hali halisi. Eneo husika awali lilikuwa ni la mradi wa Serikali wa umwagiliaji maji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wa Kata ya Mwakijembe wanaombwa wawe na subira pindi taratibu za kisheria za utwaaji wa eneo zikikamilika. Serikali italipa fidia kwa wananchi kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia sababu zilizotolewa hadi Jeshi kukabidhiwa eneo hilo, Jeshi litaendelea kutumia eneo hilo wakati taratibu za ulipwaji wa fidia zinaendelea.