Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ujenzi wa barabara ya Tabora – Mbambali – Bukene – Itobo hadi Kahama umefikia hatua gani baada ya kutengewa fedha kwenye bajeti mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 1

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina swali moja la nyongeza.

Umuhimu wa barabara hii umeongezeka baada ya ule mradi mkubwa wa bomba la mafuta kutoka Uganda mpaka Tanga, umeamua kujenga ile kambi kubwa itakayoandaa mabomba yote yatakayofukiwa njia nzima pembeni ya barabara hii na kwa kuwa wasimamizi wa mradi huu wale ECOP wana package ya miundombinu ya kuboresha barabara; na kwa kuwa kuna kakipande kama kilometa 50 mpaka 60 kutoka Nzega - Itobo mpaka kwenye ile kambi ambako mabomba yatapita.

Je, Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi haioni umuhimu wa kukaa na hawa wasimamizi wa mradi huu wa ECOP kwa sababu na wenyewe wana package ya miundombinu wakashirikiana ili kipande hiki cha kilometa 50 mpaka 60 cha Nzega - Itobo mpaka Sojo ambako ni kipande katika barabara hii hii, wakashirikiana na wakapunguza gharama upande wa Serikali na huu mradi ukatoa fedha zake ili kukamilisha barabara hii? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Selemani Zedi, Mbunge wa Bukene kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nimshukuru Mheshimiwa Zedi kwa mchango huo na mimi nimhakikishie Wizara pamoja na hawa watu wa ECOP tutakaa nao kuona uwezekano wa kujenga hiki kipande cha kilometa 50 hadi 60 kutoka Itobo hadi Nzega ili kuweza kurahisisha utengenezaji wa hili bomba, kwa hiyo mimi binafsi nimhakikishie Mheshimiwa nitafika Jimboni kwake na tuweze kuangalia uwezekano huo, ahsante.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ujenzi wa barabara ya Tabora – Mbambali – Bukene – Itobo hadi Kahama umefikia hatua gani baada ya kutengewa fedha kwenye bajeti mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru; kwa kuwa viongozi wa Kitaifa waliahidi pale Makambako kutengeneza barabara kilometa mbili za lami pale mjini. Ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ya viongozi wa Kitaifa? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama alivyosema sisi kama Wizara na Serikali kazi yetu kwakweli ni kuhakikisha kwamba zile ahadi zote zilizoahidiwa na viongozi wa chama na hasa ngazi ya kitaifa zinatekelezwa, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Deo Sanga, Mbunge wa Makambako ahadi hizo zitatekelezwa kulingana na fedha zitakapoendelea kupatikana na hasa katika kipindi hiki cha miaka mitano ambacho ndicho tumekianza, ahsante. (Makofi)

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: - Je, ujenzi wa barabara ya Tabora – Mbambali – Bukene – Itobo hadi Kahama umefikia hatua gani baada ya kutengewa fedha kwenye bajeti mwaka 2020/2021?

Supplementary Question 3

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniona nilitaka kuulizwa swali la nyongeza kwamba viporo vya barabara zinazounganisha mikoa ni pamoja na viporo vya barabara ya eneo la Malagalasi - Uvinza kilometa 51 na kiporo cha barabara inayotoka Tabora kuja Nguruka kilometa 40; nataka nijue Serikali ni lini ujenzi wa viporo hivi kukamilisha barabara inayounganisha Mkoa wa Kigoma na Tabora vitakamilika? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kilumbe Ng’enda, Mbunge wa Kigoma Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara alizozitaja za Kaliua mpaka Chagu yenye kilometa kama 36 tayari mkandarasi yupo site na amepiga kambi Kijiji cha Usinge, kwa hiyo ujenzi unaanza, lakini katika barabara ambazo zimetangazwa mwezi huu ambazo zinafadhiliwa na Mfuko wa OPEC kutoka Malagalasi hadi Uvinza yenye kilometa 51.3 tayari barabara hii imeshatangazwa kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi kwa kiwango la lami na hivyo Mheshimiwa Kilumbe na wananchi wa Kigoma baada ya muda si mrefu kuanzia Dodoma mpaka Kigoma itakuwa ni kwa lami tu bila kugusana na vumbi, ahsante. (Makofi)