Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 56 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 472 2021-06-22

Name

Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Primary Question

MHE. SELEMANI J. ZEDI aliuliza: -

Je, ujenzi wa barabara ya Tabora – Mbambali – Bukene – Itobo hadi Kahama umefikia hatua gani baada ya kutengewa fedha kwenye bajeti mwaka 2020/2021?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Selemani Jumanne Zedi, Mbunge wa Bukene, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imekamilisha kazi ya upembuzi yakinifu, usanifu wa kina na utayarishaji wa makabrasha ya zabuni kwa ajili ya ujenzi wa barabara ya Tabora – Mbambali – Bukene – Itobo yenye urefu wa kilometa 114. Kazi hii ilitekelezwa na Mhandisi Mshauri NIMETA Consult ya Tanzania na ilikamilika Aprili, 2020 kwa gharama ya shilingi milioni 790.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya shilingi milioni 1,000 sawa na bilioni moja zimetengwa kwa ajili ya kuanza maandalizi ya ujenzi wa barabara hii kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Spika, aidha, wakati Serikali inaendelea na maandalizi ya kuanzia ujenzi wa barabara hii, Wizara yangu kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) inaendelea kuifanyia matengenezo mbalimbali ili iendelee kupitika majira yote ya mwaka. Ahsante. (Makofi)