Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Primary Question

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bonde la Ruvu linatumika kwa kilimo cha umwagiliaji ili kukabiliana na changamoto ya usalama wa chakula?

Supplementary Question 1

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri yaliyotolewa na Serikali, lakini ninataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri; sasa ni lini Serikali itakuja na mkakati ulio mzuri zaidi ukiangalia kwamba maji yanayopotea katika bonde lile ni mengi sana na ile tija ya kilimo haipatikani katika lile ambalo tunaita usalama wa chakula katika nchi yetu?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Ridhiwani.

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba utilization level ya Ruvu na mito mingine mikubwa katika nchi yetu haijafikiwa kiwango ambacho tunakitarajia na tunacho-expect, lakini hatua tulizochukua sasa hivi katika mpango wa umwagiliaji wa mwaka 2018 ambao tumeuandaa kama Wizara na hivi karibini chini ya uongozi wa Mheshimiwa Waziri Mkuu alitoa maelekezo ambayo tumekaa na Wizara ya Fedha kwa ajili ya kubadilisha model za financing za umwagiliaji na sasa tunaelekea kwenye mfumo wa EPC ambayo tutafanya miradi mikubwa ya kielelezo kwa ajili ya kuchagua maeneo machache na kuweza kuyapa kipaumbele na moja ya eneo ni Mto Ruvu na Mto Ruvuma.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bonde la Ruvu linatumika kwa kilimo cha umwagiliaji ili kukabiliana na changamoto ya usalama wa chakula?

Supplementary Question 2

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naitwa Michael Constantine Mwakamo, Mbunge wa Kibaha Vijijini.

Naomba niulize swali la nyongeza; kwa kuwa Kibaha Vijijini kuna scheme ambayo inaendelea kujengwa lakini hijaaza uzalishaji na tatizo kubwa ni mifugo kuingia na kufanya uharibifu.

Je, Serikali itatusaidiaje kuondoa tatizo hilo kuhamisha wafugaji wale kwenda kwenye eneo la ufugaji la NARCO ili wakulima wa eneo lile walime kwa uhakika? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Kibaha Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa hili ni jambo specific na ni jambo linahusu sehemu moja, nitamuomba baada ya hapa tukae tukutane ili tukae na wenzetu wa Wizara ya Mifugo ili tuweze kulijadili na kulitatua kw apamoja. (Makofi)

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bonde la Ruvu linatumika kwa kilimo cha umwagiliaji ili kukabiliana na changamoto ya usalama wa chakula?

Supplementary Question 3

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, katika maeneo ambayo ameyasema Waziri kwamba yatajengewa scheme za uhakika, sikumsikia akitaja eneo la Ruvu Tambarare ya Same na Mto Ruvu huwa unaharibu sana eneo hilo. Je, ni lini sasa Serikali itawajengea watu wale scheme ya uhakika? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la mama yangu, Mama Shally kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, sijataja maeneo ya Mkoa wa Tanga, Kilimanjaro; ni moja ya maeneo ambayo ni potential, kwa hiyo nawaomba tu Waheshimiwa Wabunge waweze kutuvumilia, tumeunza huu mchakato na wenzetu wa Wizara ya Fedha na baada ya bajeti tutakuwa tuna kikao cha pamoja kwa ajili ya kuchagua maeneo yote ambayo yatakuwa ni ya miradi ya kielelezo katika umwagiliaji. Kwa hiyo, kila ambapo kuna potential na upande wa Kaskazini ni eneo muhimu sana kwetu kwa ajili ya uzalishaji. (Makofi)