Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 56 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 468 2021-06-22

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Primary Question

MHE. RIDHIWANI J. KIKWETE aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha Bonde la Ruvu linatumika kwa kilimo cha umwagiliaji ili kukabiliana na changamoto ya usalama wa chakula?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ridhiwani Jakaya Kikwete Mbunge wa Jimbo la Chalinze kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Bonde la Ruvu ni moja kati ya mabonde yanayofaa kwa kilimo cha umwagiliaji ambacho kinasaidia uhakika wa chakula na kukabiliana na changamoto ya usalama wa chakula. Serikali imeianisha takribani skimu 21 zenye eneo la ukubwa wa takribani hekta 85,075 zinazofaa kwa kilimo cha umwagiliaji katika Bonde la Ruvu katika Mikoa ya Morogoro na Pwani. Aidha, jumla ya hekta 1,284 zimeendelezwa kwa kuwekewa miundombinu ya umwagiliaji na wakulima wanatumia eneo hilo kwa ajili ya uzalishaji wa mazao ya kilimo.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Tume ya Taifa ya Umwagiliaji imepanga kuendeleza ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya umwagiliaji katika skimu zote zilizopo katika Bonde la Ruvu kama zilivyoainishwa kwenye Mpango wa Maendeleo wa Umwagiliaji wa mwaka 2018. Aidha, utekelezaji wa mpango huo umeshaanza katika skimu za Tulo (Morogoro DC), Msoga (Bagamoyo DC), Kwala (Kibaha DC) na Bagamoyo.