Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:- Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Sumbawanga katika Mji wa Laela baada ya agizo la Serikali la kuhamisha Makao Makuu?

Supplementary Question 1

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunip nafasi hii kuuliza swali la nyongeza. Kwanza niipongeze Serikali kwa kutupelea hiyo fedha shilingi bilioni moja. Nataka kujua sasa je, ni commitment gani ya Serikali kumalizia hizo fedha shilingi bilioni 1.7 ambazo zimebaki ili jengo hilo likamilike kwa kuwa wafanyakazi wa pale katika Halmashauri yangu wanafanya kazi katika mazingira magumu sana?

Swali la pili, kwa kuwa ujenzi wa Ofisi ya Mkurugenzi ni component inaenda pamoja na ujenzi wa nyumba ya watumishi ikiwemo nyumba ya Mkurugenzi na Wakuu wa Idara. Nataka kujua je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha jambo hilo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Kwela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwanza nipokee pongezi zake kwa Serikali kwa kupeleka shilingi bilioni moja, lakini commitment ya Serikali tayari imetenga shilingi bilioni moja nyingine kwenye mwaka wa fedha 2021/2022 na shilingi bilioni moja tayari ipo Halmashauri ya Sumbawanga na kazi inaanza siku hii ya leo. Kwa hiyo, nimhakikishie kwa mtiririko huu, Serikali itaendelea kutenga fedha kuhakikisha tunakamilisha jengo la utawala katika Halmashauri ya Sumbawanga.

Mheshimiwa Spika, lakini pili, mpango wa ujenzi wa majengo ya utawala unaenda sambamba na mipango ya ujenzi wa nyumba ya watumishi kwa maana ya Mkurugenzi na Wakuu wa Idara. Kwa hiyo, safari ni hatua nimhakikishie wakati tunaendelea na ujenzi wa jengo la utawala pia tunakwenda kuweka mipango ya kuanza ujenzi wa nyumba za Mkurugenzi na Wakuu wa Idara kwa awamu, ahsante sana.