Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 56 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 465 2021-06-22

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. DEUS C. SANGU aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya Halmashauri ya Sumbawanga katika Mji wa Laela baada ya agizo la Serikali la kuhamisha Makao Makuu?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deus Clement Sangu, Mbunge wa Jimbo la Kwela kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ni miongoni mwa Halmashauri 30 zilizohamia kwenye maeneo mapya ya utawala mwaka 2019.

Mheshimiwa Spika, ili kuwezesha Halmashauri kutoa huduma bora kwa wananchi, Serikali imeweka mpango wa ujenzi wa jengo la utawala utakaogharimu shilingi bilioni 2.7.

Mheshimiwa Spika, mwezi Mei, 2021 Serikali imeipatia Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuanza ujenzi. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi bilioni moja kwa ajili ya kuendelea na ujenzi huo. Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga imesaini mkataba wa ufundi na Chuo cha Sayansi Mbeya kwa ajili ya ujenzi utakaoanza tarehe 22 Juni, 2021.

Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kutenga fedha za ukamilishaji wa jengo hilo, ahsante sana.