Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: - (a) Je, ni asilimia ngapi ya mapato yatokanayo na Uvuvi wa Bahari Kuu yanaenda upande wa Zanzibar? (b) Je, kwa miaka mitano iliyopita Zanzibar imepata kiasi gani?

Supplementary Question 1

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Nimshukuru pia kaka yangu, Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa majibu mazuri yanayoridhisha na kutia moyo. Hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza; kwa kuwa kipato hicho ni kidogo, Serikali ina mpango gani wa kuongeza pato hili kwa pande zote mbili za Muungano na kuwasaidia wavuvi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili; kwa kuwa mgawanyo wa mapato ni wa kisheria, je, Wizara inawasaidiaje wavuvi kutoka Zanzibar wanaoleta samaki bara na wale wanaopeleka mifugo Zanzibar ili kuondoa kero na usumbufu unaowapata? Ahsante. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ni jitihada gani za Serikali zinafanywa kuongeza pato hili kwa kuwa pato hili ni dogo. Kwanza naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge wote na Watanzania kwa ujumla, natoa shukrani nyingi sana kwa Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Sita, Mama Samia Suluhu Hassan na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Nane, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, kwa kuridhia mabadiliko ya sheria na kanuni ambazo zimekwenda sasa kufungua mwanya wa uwekezaji zaidi katika uvuvi wa bahari kuu. Hivi ninavyozungumza, tayari makampuni takribani 20 yameshakata leseni na kuingiza pato la zaidi ya shilingi bilioni moja kwa Mamlaka ya Uvuvi wa Bahari Kuu; ni jitihada kubwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, jitihada nyingine ambayo Serikali hizi mbili zimefanya ni kuhakikisha kwamba tunaweka kipengele ya uvutiaji kwa maana ya incentive. Tumeshatoa maelekezo kwa Mamlaka yetu ya Uvuvi wa Bahari Kuu kuitisha kikao ambacho kitatusaidia kuwaunganisha wadau wote kwa lengo la kwamba tuvitambue sasa vile vivutio ambapo tutawapa Waheshimiwa Mawaziri wawili; wa Jamhuri na yule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, waweze kuvitangaza hadharani ili wawekezaji wajue iko fursa gani ya kuweza kuwekeza zaidi katika uvuvi wa bahari kuu.

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la pili, baada ya hili la kuongeza kipato, ni nini tunafanya kuondoa vikwazo. Mambo makubwa mawili yanafanyika; hivi sasa timu zetu za wataalam kutoka Zanzibar na kutoka Bara zinakaa pamoja kujadili mambo makubwa mawili; la kwanza, ni leseni za wavuvi wa Zanzibar ziweze kufanya kazi hata huku Bara pia, lakini la pili ni kuondoa kikwazo kile cha mifugo inayotoka Bara kwenda Zanzibar na kulipiwa ushuru mkubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tupo katika hatua nzuri baada ya Wakurugenzi hawa kumaliza, watakaa Makatibu Wakuu na baadaye watakaa Waheshimiwa Mawaziri ili kufanya harmonization ya sheria hizi na hatimaye Watanzania wote wa Bara na Visiwani, waweze ku-enjoy rasilimali za Taifa letu. (Makofi)