Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 55 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Waziri wa Mifugo na Uvuvi 463 2021-06-21

Name

Angelina Adam Malembeka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANGELINA ADAM MALEMBEKA aliuliza: -

(a) Je, ni asilimia ngapi ya mapato yatokanayo na Uvuvi wa Bahari Kuu yanaenda upande wa Zanzibar?

(b) Je, kwa miaka mitano iliyopita Zanzibar imepata kiasi gani?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI alijibu:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Angelina Adam Malembeka, Mbunge wa Viti Maalum, lenye vipengele (a) na (b), kama ifuatavyo: -

(a) Mheshimiwa Spika, mgawanyo wa mapato yatokanayo na uvuvi wa Bahari Kuu unafanyika kwa mujibu wa Sheria ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu Na. 5 ya mwaka 2020, Kifungu cha 79, ambayo inaelekeza mgawanyo wa mapato yanayokusanywa na Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu kwa utaratibu ufuatao, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar asilimia 20; Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania asilimia 30; na Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi Bahari Kuu asilimia 50.

(b) Mheshimiwa Naibu Spika, katika kipindi cha miaka mitano iliyopita, Mamlaka ya Kusimamia Uvuvi wa Bahari Kuu ilikusanya jumla ya Dola za Kimarekani 1,352,107.50 sawa na Sh.3,091,837,178.10. Kutokana na makusanyo hayo na kwa kuzingatia maelezo yangu katika kipengele (a), Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kufikia mwezi Machi, 2021 imepata mgao wa Sh.618,367,435.62.