Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa Barabara ya Redio Habari Maalum kwenda Hospitali ya Wilaya ya Olturumet kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa barabara hii iliahidiwa na Mheshimiwa Rais na umepita muda mrefu sana, na wananchi wamekuwa wakihoji, na katika majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri sijaona commitment. Je, ni lini hasa fedha zitapatikana kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa tunakwenda kuahirisha Bunge keshokutwa na wananchi wamekuwa wakiniuliza kila siku na kila saa kwa sababu hospitali hiyo inatumiwa na wagonjwa wengi sana kwenda kwenye hospitali ya wilaya. Ni nini nitakwenda kuwaambia wananchi wa Jimbo la Arumeru Magharibu nitakaporudi Jimboni?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali madogo mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Naibu Spika, ameuliza tu kwamba lini hasa fedha zitapatikana kwa sababu ahadi hii ni ya muda mrefu, na katika jibu letu la msingi tumeeleza hapa kwamba mara fedha zitakapopatikana basi barabara hii tutaiingiza katika mipango yetu ya kujengewa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, na kwa kuwa Serikali ilisikia kelele ama maombi ya Wabunge ambayo waliyatoa katika Bunge lako Tukufu na kusababisha Serikali kutaka kuanzisha chanzo kipya cha fedha ili TARURA iweze kuongezewa, ninaamini tutakavyopata ongezeko la fedha hiyo tutazingatia ombi la Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ameuliza ni nini akawaambie wananchi. Akawaambie tu wananchi kwamba ahadi ambayo viongozi wetu wakubwa waliitoa itatekelezwa mara hapo fedha itakapopatikana. Ahsante.