Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 55 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 457 2021-06-21

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa Barabara ya Redio Habari Maalum kwenda Hospitali ya Wilaya ya Olturumet kwa kiwango cha lami?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Barabara ya Redio Habari Maalum hadi Hospitali ya Wilaya ya Olturumet iliyopo Arumeru Magharibi yenye urefu wa kilomita 2.5 ni miongoni mwa miradi nchini ambayo ni ahadi za Rais. Serikali inaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga barabra hiyo kwa kiwango cha lami, na itatoa kipaumbele cha ujenzi pindi fedha za ujenzi zitakapopatikana.

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali imeendelea kuifanyia matengenezo barabara hii kila mwaka wa fedha ili kuhakikisha inapitika majira yote ya mwaka. Katika Mwaka wa Fedha 2019/2020 na 2020/2021 Serikali imetoa shilingi milioni 37.7 kwa ajili ya matengenezo ya barabara hiyo. Aidha, katika Mwaka wa Fedha 2021/2022 Serikali imetenga shilingi milioni 56.75 kwa ajili ya matengenezo ya barabara ya Redio Habari Maalum hadi Hospitali ya Wilaya ya Olturumet.