Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:- Je, ni lini wananchi wa Makambako watalipwa fidia baada ya maeneo yao kuchukuliwa na Serikali kwa ajili yakuzalisha umeme wa upepo?

Supplementary Question 1

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru. Nina maswali madogo mawili. Swali la kwanza; pamoja na majibu mazuri ya Serikali yenye kutia matumaini, kwa wananchi wanaopitiwa na mradi huo, wananchi wa eneo la Kivavi na eneo la Majengo na kwa sababu, wamesubiri kwa muda mrefu sana zaidi ya miaka saba na huu sasa tunakwenda mwaka wa nane. Je, Serikali itakuwa tayari kusimamia kama ambavyo wamesema hapa, ndani ya mwaka 2021/2022 na kuhakikisha kwamba, wananchi hawa watalipwa kama ambavyo amesema kwenye jibu la msingi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; je, Serikali itasimamia namna ya kuwalipa fidia wakati wa kuwalipa utakapofika? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako, kwa pamoja, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika juhudi za Serikali za kuhakikisha inaongeza wigo wa umeme, tunazalisha umeme kutoka katika vyanzo mbalimbali ikiwa ni pamoja na maji, mafuta na gesi ambayo imezoeleka. Hata hivyo, tunafanya vitu vinavyoitwa energy mix, ambavyo ni vile vyanzo jadidifu tunaviita renewables ambayo kuna upepo, jua na ile wanayoita joto ardhi. Sasa, kwenye eneo la Makambako imeonekana tunaweza tukapata pale, umeme kwa kutumia upepo katika hicho Kijiji cha Majengo tulichokisema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inatarajia kupata kama megawati 1,179 kutoka kwenye hizo renewables. Sasa, tumewakaribisha wawekezaji binafsi ili waweze kuwekeza katika eneo hilo ili isaidiane na Serikali katika kupatikana kwa umeme huo. Huo mkataba nilioutaja unaelekeza kwamba, yule mwekezaji binafsi anayekuja kuwekeza katika eneo hilo, yeye ndiye ata-acquire ardhi na kuweza kulipa fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa, nipende kutoa commitment ya Serikali, Mheshimiwa Deo amefuatilia sana kwa muda mrefu madai haya na malipo haya, nimhakikishie kwamba, tumefikia mwisho wa makubaliano na kutafuta wawekezaji katika eneo hili na Serikali itasimamia kwa asilimia 100.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, kuhakikisha kwamba, mkataba unaingiwa katika kipindi hicho kilichotajwa. Pili, kuhakikisha kwamba, kila yule anayetakiwa kulipwa fidia analipwa fidia stahiki katika eneo lake, kulingana na hali halisi na sheria inavyoelekeza katika maeneo hayo. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Deo kwamba, wananchi wa Makambako wamefanikiwa na naendelea kuwasimamia vyema na kile wanachokistahili kukipata, watakipata kwa wakati. (Makofi)