Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 54 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 454 2021-06-18

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. DEO K. SANGA aliuliza:-

Je, ni lini wananchi wa Makambako watalipwa fidia baada ya maeneo yao kuchukuliwa na Serikali kwa ajili yakuzalisha umeme wa upepo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Deo Kasenyenda Sanga, Mbunge wa Makambako, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika juhudi za kuongeza upatikanaji wa umeme nchini kupitia vyanzo mbalimbali, eneo la Kijiji cha Majengo Jijini Makambako, limebainika kuwa na uwezo wa kuwekewa miundombinu ya kuzalisha umeme kupitia nishati ya upepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inakamilisha taratibu za kuingia Mkataba wa uzalishaji wa umeme wa upepo na Mwekezaji Binafsi aitwaye Sin Tan. Kwa mujibu wa Mkataba huo, fidia kwa wananchi wa maeneo yatakayotumika kuzalisha umeme huo, italipwa na mwekezaji huyo, katika kipindi cha kuanzia mwezi Agosti, 2021 na Julai, 2022 ambacho ni kipindi kinachotarajiwa kutekelezwa kwa mradi huo.