Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:- Je ni chombo gani kinasaidia abiria kupata haki yake pindi abiria anapopata ajali safarini?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa ajali inapotokea wamiliki wa vyombo vya moto hupewa mara moja bima yao wanapokwenda kudai chombo kama imeharibika, lakini hawa waathirika ambao ni abiria wanaopata ajali wamepoteza maisha au viungo wamekuwa wakisumbuliwa sana na hawa bima.

Je, nini kauli ya Serikali kutokana na usumbufu mkubwa sana wanaopata abiria wanaopata ajali barabarani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa abiria wengi sana wanaotumia vyombo vya moto wanapopata ajali wanakuwa hawana uelewa wa kutosha na mara nyingi sana sasa hivi tumetumia electronic ticketing yaani kule nyuma hakuna elimu yoyote.

Je, sasa Serikali haioni ni wakati sasa wa kuhakikisha kwamba katika vituo vya kusubiria abiria kuwepo na mabango na matangazo ili kutoa elimu ya kutosha kwa abiria wanapopata ajali nini wafanye? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ritta Kabati, Mbunge wa Viti Maalum kutoka Iringa.

Kwanza nataka nichukue fursa hii nimpongeze sana kwa kazi nzuri ambayo anaifanya katika Mkoa wake. Mheshimiwa Ritta amefika hatua ya kukarabati Kituo cha Polisi na ujenzi wa kumalizia Kituo cha Polisi katika Kata ya Semtema. Hakika amefanya kazi kubwa, kwa hili nampongeza sana lakini na wengine pia watusaidie kufanya hiki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niombe kujibu maswali mawili. Inapotokea ajali ni kweli mmiliki wa chombo anapata fidia kama amejiunga ama amejihusisha na bima, lakini je vipi kuhusu sasa hawa abiria. Ni kweli hii ni changamoto na bado kuna changamoto nyingine kwa upande wa wananchi. Hapo nataka niwaambie kitu kwamba changamoto ya kwanza wanapopata ajali wanakuwa hawajui namna bora ya uandishi wa barua za kuombea zile fidia zao, kitu ambacho mwisho wa siku kinakuja kuwafanya wao aidha kuchelewa au kukosa kabisa kuweza kupata zile fidia kutoka bima.

Mheshimiwa Mwenyekiti, changamoto nyingine kwa kweli ipo kwenye upelelezi kwamba wale watu wa bima hawawezi kutoa zile fedha za fidia unless mpaka wahakikishe kwamba wamepata attachment ya upelelezi kutoka Jeshi la Polisi. Kwa hiyo, hapo nataka nitoe wito pia kwa Jeshi la Polisi kwamba wahakikishe wanafanya haraka kupeleka ripoti za upelelezi kwa hawa wananchi ambao wanapata ajali ili sasa waweze kupata fidia zao kwa haraka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kikubwa zaidi uelewa mdogo wa hii taaluma ya bima. Hapa natala nitoe agizo kwa Jeshi la Polisi, kwamba pamoja na kazi nzuri ya utoaji wa elimu kwa wananchi juu ya namna bora ya utumiaji wa barabara, lakini suala la elimu hii ya bima ya kuweza kupata mafao iendelee na kazi ifanyike vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine alikuwa anauliza je, sasa tuna mpango gani wa kuweka haya mabango.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mabango yapo, kazi imeanza na inaendelea, lakini kingine tunaendeleza taaluma ambazo kupitia mabango, vyombo vya habari, vijiwe vya bodaboda, shule pamoja na kupitia kila mahala; tunawaelewesha watu namna bora ya kutumia barabara na kuepuka na ajali. Kikubwa zaidi tumeshaweka ishara na alama za barabarani ambazo pia zinasaidia watu kuweza kujua namna ya kuepuka hizi ajali za barabarani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.