Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 54 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 450 2021-06-18

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza:-

Je ni chombo gani kinasaidia abiria kupata haki yake pindi abiria anapopata ajali safarini?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Ritta Enespher Kabati, Mbunge Wa Viti Maalumu kutoka Iringa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtu au watu wanaopata ajali au madhara kutokana na chombo cha moto ambacho fidia yake inasimamiwa na Sheria ya Bima wanapaswa kulipwa fidia ya madhara waliyoyapata ama kwa kuumia au kifo kutoka kwenye kampuni ya bima ambayo chombo hicho cha moto kimekatia bima yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya ajali kutokea tukio hukaguliwa na Askari wa Kikosi cha Usalama Barabarani na wahanga wa ajali hupatiwa fomu ya matibabu. Taarifa ya ajali fomu hii hupelekwa ofisi za bima husika na kwa mmiliki wa chombo cha moto kilichopata ajali. Kisha shauri la ajali hupelekwa mahakamani na kesi ikimalizika fomu namba 115 hutolewa kuonyesha matokeo ya kesi (Final Case Report). Ndipo wahanga wa ajali au ndugu huchukua nyaraka za ramani ya tukio la ajali, fomu ya matibabu, fomu ya taarifa ya ajali, fomu ya matokeo ya kesi, fomu ya ukaguzi wa chombo kilichofanya ajali, taarifa ya uchunguzi wa marehemu, kama mhanga amefariki na nakala ya bima ya gari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nyaraka zote hizo hupelekwa kwenye kampuni ya bima ambayo chombo cha moto kilichohusika na ajali kimekatia bima yake na wahanga hufidiwa kutokana na ukubwa wa madhara waliyoyapata. Kwa ufupi Jeshi la Polisi linathibitisha kutokea kwa ajali, Mahakama inatafsiri sheria kuhusu tukio, Daktari anathibitisha madhara waliyopata wahanga na kampuni ya bima inalipa fidia. Ninakushukuru.