Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha huduma ya Maji kwa Wananchi wa Kata za Kipatimu, Kibata, Chumo, Kandawale, Namayuni, Miguruwe, Njinjo, Mitole na Kinjimbi katika Jimbo la Kilwa Kaskazini ili kuwaondolea adha ya maji inayowakabili?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu namba moja la nyongeza ningependa kufahamu, kwa kuwa katika Mikoa ya Kusini kumekuwa na vyanzo vingi vya maji vinavyotokana na mito mikubwa kama ule wa Rufiji, Ruvuma, Mavuji, Lukuledi, Luhuhu pamoja na Ketewaka kule Njombe. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kwamba inamaliza tatizo la maji kwa asilimia 100 kama ilivyofanyika Kanda ya Ziwa kupitia vyanzo hivi vya maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Ndulane kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, awali ya yote napenda sana kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji mzuri. Nipende tu kumjibu swali lake la nyongeza la matumizi ya maji yote yanayopatikana kwenye mito na vyanzo vyote vikubwa vyenye uhakika kwa miradi endelevu. Sisi kama Wizara, mikakati yetu katika mwaka ujao wa fedha na kuendelea, ni kujenga miradi mikubwa inayofanana na mradi huu wa Ziwa Viktoria. Mikakati imekamilika na kwa Kusini pia tumepanga kutumia Mto Ruvuma, Mto Rufiji na Ziwa Tanganyika. Hii yote tutakuja kuitekeleza kadri tutakavyokuwa tukipata fedha. (Makofi)

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Je, ni lini Serikali itafikisha huduma ya Maji kwa Wananchi wa Kata za Kipatimu, Kibata, Chumo, Kandawale, Namayuni, Miguruwe, Njinjo, Mitole na Kinjimbi katika Jimbo la Kilwa Kaskazini ili kuwaondolea adha ya maji inayowakabili?

Supplementary Question 2

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipatia nafasi hii. Naomba kuuliza swali moja la nyongeza kwamba, katika Jimbo la Newala Vijijini, kuna Mradi wa Maji wa Mnima Miuyu, mradi huu ulikuwa ni wa miezi tisa, ulikuwa ni mwaka 2018 na hadi leo hii haujakamilika. Je, ni lini mradi huu utakamilika ili wananchi wa Jimbo la Newala Vijijini waweze kupata maji ya uhakika? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Naibu Spika ahsante. Naomba kujibu swali la Mbunge wa Jimbo la Newala Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, miradi yote ambayo utekelezaji wake umeanza na ipo katika process, yote lazima itakamilika kadri fedha tunavyozipata na kadri ya muda ulivyopangwa. Hivyo nipende kumtoa hofu Mheshimiwa Mbunge, namna ambavyo amekuwa akizungumza nasi mara kwa mara, tuendelee kuwasiliana kwa karibu na tutakwenda pia kuona kazi imefikia wapi na kazi itakamilika kadiri inavyotakiwa.