Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 53 Water and Irrigation Wizara ya Maji 444 2021-06-17

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itafikisha huduma ya Maji kwa Wananchi wa Kata za Kipatimu, Kibata, Chumo, Kandawale, Namayuni, Miguruwe, Njinjo, Mitole na Kinjimbi katika Jimbo la Kilwa Kaskazini ili kuwaondolea adha ya maji inayowakabili?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis K. Ndulane, Mbunge wa Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, katika Mwaka wa Fedha 2020/2021 Serikali imeendelea kuboresha huduma ya maji kwa kutekeleza miradi Wilayani Kilwa ambayo imehusisha uchimbaji wa visima virefu nane, ukarabati wa tanki la maji la lita 45,000 katika Kijiji cha Kipatimu, ukarabati wa mradi wa maji Mtubei Mpopera katika Kata ya Kandawale na ujenzi wa vituo 11 vya kuchotea maji. Kukamilika kwa kazi hizo kumeboresha upatikanaji wa huduma ya maji kufikia asilimia 68.5.

Mheshimiwa Naibu Spika katika Mwaka wa Fedha 2021/2022, Serikali itaendelea kuboresha huduma ya maji safi na salama na yenye kutosheleza katika Wilaya ya Kilwa kwa kutekeleza miradi mbalimbali ya maji ikiwemo uchimbaji wa visima virefu sita katika Vijiji vya Mitole Kata ya Mitole, Zinga kibaoni Kata ya Miguruwe, Namayuni Kata ya Namayuni, Kisima-Mkika Kata ya Njinjo, Kibata Kata ya Kibata na Ruhatwe Kata ya Kikore. Pia, ujenzi wa miradi mitano ya mitandao ya mabomba ya matanki ya kuhifadhia maji katika Vijiji vya Kinjimbi Kata ya Kinjimbi, Chapita Kata ya Migumbi, Chumo Kata Chumo, Marendego Kata ya Somanga na Kipindimbi Kata ya Njinjo. Aidha, katika vijiji hivyo kutajengwa vituo 50 vya kuchotea maji.