Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, lini Serikali sasa itaipandisha Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kuwa Wilaya kamili?

Supplementary Question 1

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwa kuwa Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala yapo katika Kata ya Ntobo na ukizingatia Kata zake zilivyokuwa mbalimbali hususan Kata za Isaka, Mwalugulu, Jana na Mwakata kupata taabu sana kupata huduma za ki- Halmashauri. Sasa nini mpango wa Serikali wa kuanzisha Mamlaka ya Mji mdogo katika Kata ya Isaka ili kuwawezesha wana Isaka nao sasa waweze kupata huduma kwa urahisi. Ahsante sana. (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Kassim Iddi Iddi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Mbunge ameomba tu kwamba kwa nini sasa Serikali isianzishe Mamlaka ya Mji Mdogo katika eneo la Makao Makuu ya Halmashauri ya Msalala kwenye Kata ya Ntobo kama alivyoeleza. Kwa hiyo, ametaka kujua ni lini lakini jibu langu la msingi utaratibu ni uleule kwamba mkitaka tuanzishe haya Mamlaka maana yake mfuate taratibu hizi ambazo tumezianisha, mlete maoni yapitie katika ngazi zote na sisi tutafanya tafakuri na tathmini na baadae tukishajiridhisha basi maomba hayo tutayapeleka kwa Mheshimiwa Rais ambaye ndiye ana mamlaka ya mwisho kabisa ya kutangaza maeneo hayo.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, hilo ndilo jibu la Serikali anzisheni mchakato nasi tutakuja tufanye tathmini. Ahsante.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: - Je, lini Serikali sasa itaipandisha Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kuwa Wilaya kamili?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuuliza Mamlaka ya Mji wa Vwawa inahudumia Mkoa wa Songwe. Je, ni lini Serikali itaupandisha hadhi Mamlaka ya Mji wa Vwawa kuwa Halmashauri ya Mji.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Hasunga, Mbunge wa Vwawa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikushukuru sana kwa kunisaidia kujibu. Kikubwa ni kwamba kwanza na mimi mwenyewe nina interest kwa sababu natokea katika Mkoa huo huo wa Songwe na ninaufahamu vizuri Mji Mdogo wa Vwawa ambao unahudumia kwa sasa Makao Makuu ya Mkoa wetu wa Songwe.

Kwa hiyo, kikubwa mimi na wewe pamoja na Mkuu wa Mkoa wetu ambaye anatusikia sasa hivi nafikiri tuanzishe tu mchakato mapema halafu ikishafika katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI ninaamini tuki-meet vigezo vyote basi tutafanya hilo ambalo Mheshimiwa Mbunge ameliomba, ahsante.