Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 53 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 440 2021-06-17

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. IDDI K. IDDI aliuliza: -

Je, lini Serikali sasa itaipandisha Halmashauri ya Wilaya ya Msalala kuwa Wilaya kamili?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kassim Iddi Iddi, Mbunge wa Jimbo la Msalala kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, utaratibu wa kuanzisha Mkoa na Wilaya mpya umebainishwa kupitia Sheria ya Uanzishwaji wa Mikoa na Wilaya. Kwa mujibu wa Sheria hii, utaratibu wa kuanzisha Wilaya mpya huanzia kwenye Serikali za Vijiji/Mitaa ili kupata ridhaa ya wananchi kisha hupelekwa kwenye Mabaraza ya Madiwani ya Halmashauri, Kamati ya Ushauri ya Wilaya (DCC) na Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC). Baada ya hatua hiyo, maombi hayo huwasilishwa Ofisi ya Rais – TAMISEMI kwa ajili ya uhakiki na kujiridhisha na baadaye kuwasilishwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili akiridhia atoe kibali cha kuanzishwa kwa Wilaya husika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri ya Wilaya ya Msalala iko katika Wilaya ya Kahama ambayo ni moja kati ya Wilaya tano zinazounda Mkoa wa Shinyanga. Halmashauri ya Wilaya ya Msalala bado haijaanza mchakato wa kuomba kuwa Wilaya kwa kadri ya matakwa ya sheria.