Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Uhamiaji katika Kijiji cha Chikongo kilichopo Kata ya Moreha Wilayani Tandahimba ambacho huduma ya Visa kwa Watanzania waendao Msumbiji hutolewa?

Supplementary Question 1

MHE. KATANI A. KATANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, majibu ya Serikali nadhani haielewi Swali langu la Msingi. Chikongo tunaposema upande wa pili wa Msumbiji, wenzetu tayari wanacho kituo cha uhamiaji, upande wa Tanzania ndio hatuna kituo cha uhamiaji: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa swali languni kwamba, ni lini Serikali itapeleka kituo cha uhamiaji upande huu wa Tanzania? Si suala la mashauriano na Msumbiji kwa sababu, Msumbiji wao tayari wanacho kituo cha uhamiaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali la pili. Je, wenzetu wa Msumbiji tunapopeleka bidhaa kule wana custom pale, wana shughuli zote pale. Upande wa Tanzania wananchi wetu wakileta bidhaa wanapata shida kwa sababu hawana custom hapo, TRA hawapo pale. Tupe kauli ya Serikali, ni lini mtajenga kituo cha uhamiaji pale na kupeleka huduma nyingine zote za msingi ili Watanzania wapate huduma kwa urahisi pale?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Katani, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niruhusu nimpongeze sana Mheshimiwa Katani kwa kazi nzuri anayoifanya; na ndiyo maana wananchi wa Tandahimba walimuamini na kumpa nafasi ya kuwawakilisha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme kwa ujumla wake kwamba lengo la Serikali ni kudhibiti maeneo yote ya mipaka yetu, ikiwemo uingiaji wa wageni na utokaji pia wa wananchi wetu. Pia kudhibiti mapato kupitia TRA, yako pia masuala ya afya pamoja na masuala ya usalama kwa ujumla wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kuhusu maswali yake yote mawili kwa ujumla. Ni kwamba niwatoe hofu tu wananchi wa Tandahimba, tunaona uko umuhimu. Kituo cha uhamiaji ambacho tunacho kiko makao makuu ya wilaya, ni mbali kidogo na sehemu ambapo wananchi wanavuka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Katani, kwamba suala hili tumelichukua. Nitumie nafasi hii tu kumuelekeza Kamishna wa Uhamiaji atume wataalam pale. Kwa sababu wananchi kama wanagonga passport zao ng’ambo wanapoingia; ni muhimu wananchi pia wa Tanzania waweze kupata huduma vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, suala hili nalielekeza tu lifanyiwe kazi mara moja na sisi tutaendelea kusimamia kama Serikali kuona wananchi hawapati shida na tunapata manufaa makubwa sana kutoka kwa nchi za majirani kupitia biashara na mambo mengine ambayo yanahusiana na mambo ya mipakani. Ahsante sana.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Uhamiaji katika Kijiji cha Chikongo kilichopo Kata ya Moreha Wilayani Tandahimba ambacho huduma ya Visa kwa Watanzania waendao Msumbiji hutolewa?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Mimi ninauliza swali moja ambalo ni, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi kwenye Soko la Kimataifa la Mwika ambalo liko mbali sana kutoka Himo ambako ndiko kwenye kituo cha polisi?

Mheshimiwa Mwneyekiti, ahsante sana.

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, nimjibu Mheshimiwa Kimei, swali lake la nyongeza, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Kimei, kama ulivyosema, na niseme tu kwamba uko umuhimu wa kuwa na kituo cha polisi. Si maeneo tu haya ya Mwika, lakini maeneo mengi ambayo yanaweza yakawa yanajihusisha na biashara kama ilivyo eneo la Mwika. Nilichukue suala hili ili tuone upande wa Serikali kulifanyia kazi haraka ili tuweze kuleta manufaa makubwa. Ili biashara iweze kushamiri vizuri tunahitaji kwa kweli kuwa na ulinzi wa kutosha katika maeneo haya. Ahsante sana.