Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 52 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 439 2021-06-16

Name

Katani Ahmadi Katani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tandahimba

Primary Question

MHE. KATANI A. KATANI aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga Kituo cha Uhamiaji katika Kijiji cha Chikongo kilichopo Kata ya Moreha Wilayani Tandahimba ambacho huduma ya Visa kwa Watanzania waendao Msumbiji hutolewa?

Name

George Boniface Simbachawene

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibakwe

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, ninapenda kujibu swali la Mheshimiwa Katani Ahmed Katani, Mbunge wa Tandahimba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Chikongo ni eneo lilioko pembezoni mwa Mto Ruvuma katika Wilaya ya Tandahimba ambayo kwa upande wa Msumbiji inapakana na Wilaya ya Nangale. Kwa sasa huduma za uhamiaji katika Kijiji cha Chikongo zinapatikana kupitia ofisi ya Uhamiaji ya Wilaya ya Tandahimba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia Idara ya Uhamiaji itafanya mashauriano na nchi ya Msumbiji kuanzisha kituo cha uhamiaji katika eneo la Kijiji cha Chikongo kilichopo katika Wilaya ya Tandahimba ili kuendelea kutoa huduma kwa Watanzania waendao nchini Msumbiji.