Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Igunga?

Supplementary Question 1

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kwanza niipongeze Wizara, Waziri na Naibu wake wanafanya vizuri. Mwezi Januari Naibu Waziri alipita pale alifanya ziara na akatoa maelekezo mwezi wa tatu chuo kikamilike lakini nimefanya ziara Jumamosi tarehe 12 changamoto imekuwa ni kwamba fedha zinakwenda kidogo katika kukamilisha huu mradi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba commitment ya Serikali katika kukamilisha fedha ambazo zitaenda kukamilisha huu mradi na kuanza udahili. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ngassa kama ifuatavyo:

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kulikuwa na kusuasua kidogo katika kupeleka fedha zile za awamu ya mwisho kuhakikisha kwamba tunakwenda kukamilisha ujenzi katika maeneo haya. Lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, fedha awamu ya mwisho zaidi ya Shilingi milioni 560 tayari zimeshapelekwa katika chuo hiki kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi huo na tutahakikisha kwamba tunasimamia vyema kuhakikisha ujenzi huo unakamilika ifikapo Julai ili vijana wetu waweze kuanza mafunzo katika eneo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuwasilisha.

Name

Aloyce John Kamamba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buyungu

Primary Question

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Chuo cha VETA Igunga?

Supplementary Question 2

MHE. ALOYCE J. KAMAMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, uhitaji wa Chuo cha Ufundi VETA ambao unawakabili wananchi wa Wilaya ya Igunga unafanana sana na uhitaji wa chuo hicho katika Wilaya ya Kakonko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lini Serikali itajenga chuo cha ufundi VETA katika Wilaya ya Kakonko? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kamamba Mbunge wa Buyungu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuwa na Chuo cha VETA katika kila Wilaya hapa nchini. Kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko makini, kwa hivi sasa tunakamilisha ujenzi wa vyuo hivi 29 katika Wilaya hizi 29 nchini.

Baada ya awamu hii kukamilika Serikali tutajipanga vema kulingana na upatikanaji wa fedha tutahakikisha kwamba tunakwenda kujenga chuo katika kila Wilaya hapa nchini. Ahsante.