Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Katesh – Hydom kwa kiwango cha lami ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za afya katika Hospitali ya Hydom pamoja na usafirishaji wa mazao hasa ngano?

Supplementary Question 1

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

La kwanza, kwa kuwa Serikali imesema upembuzi yakinifu wa barabara ya Katesh – Hydom unakamilika Juni, yaani mwezi huu; na kwasababu mfumo wa sasa ni wa kusanifu na kujenga. Je, baada ya mwezi wa sita ambapo upembuzi utakamilika Serikali iko tayari kuanza ujenzi mara moja?

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kwenye barabara hiyo kuna maeneo mawili korofi moja ni daraja ambalo lipo Njia Panda ya Dawar kwenye hiyo barabara ya kwenda Hydom, lakini lingine ni ule Mlima Chavda ambao unakwaza usafiri na usafirishaji kwa kata za Bassodesh, Garawja, Hirbadaw, Getanuwas, Bassotu, Murbadau, Dawar yenyewe na Mogitu na mara nyingi wananchi wamekuwa wakipoteza maisha yao na kupoteza mali.

Je, Serikali itakuwa iko tayari sasa kuweka lami wakati tukitarajia ujenzi uanze kwenye eneo la Mlima Chavda na kujenga daraja imara pale kwenye ule mto uliopo kwenye njia panda ya Dawar?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Samwel Hhayuma, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna aina mbili, ya usanifu na kujenga ama kusanifu halafu baadaye kujenga. Kwa kuwa tayari tunafanya upembuzi yakinifu, itategemea na upatikanaji wa fedha kama utaruhusu tufanye utaratibu wa kusanifu na kujenga. Lakini kama fedha itakuwa haipo, kwa maana ya bajeti ya mwaka tunaoanza kutekeleza baada ya kukamilisha upembuzi yakinifu tutafanya usanifu wa kina ili barabara hiyo sasa iwe tayari kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi wa kiwango cha lami kwa hela hiyo ya mfadhili kutoka benki ya Ujerumani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kuhusu daraja na maeneo korofi tayari tulishatoa taarifa kwa mameneja wote barabara zote ambazo zina maeneo korofi waweze kuyaainisha ili tuweze kuyafanyia mkakati wa kuyatengeneza si tu kwa barabara hii ya Hydom – Katesh bali ni pamoja na barabara zote ili tuweze kuyatengeneza, hata ikiwezekana kuweka lami nyepesi ili yaweze kupitika kwa kiwango chote. Kuhusu madaraja wataalamu wako barabarani wakiwa wanaangalia uharibifu wa madaraja hayo yote na kuweza kuyatengeneza ili baada ya kipindi hiki cha mvua kukatika basi barabara zote ziweze kupitika bila kuleta bugudha. Ahsante.

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Katesh – Hydom kwa kiwango cha lami ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za afya katika Hospitali ya Hydom pamoja na usafirishaji wa mazao hasa ngano?

Supplementary Question 2

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Dareda, Bashnet na Dongobesh, kwa kuwa barabara hii inaunganisha wilaya mbili wilaya ya Mbulu na Babati lakini vile vile itaunganisha halmashauri mbili ambazo zinahamia makao mapya halmashauri ya wilaya ya Mbulu inayohamia Dongobesh na halmashauri ya wilaya ya Babati ambayo sasa inahamia Dareda? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Yustina Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo. Barabara ya Dongobesh Dareda ni barabara muhimu ambayo tayari Serikali imeshakamilisha upembuzi yakinifu na usanifu wa kina na hivyo Serikali kwa sasa inatafuta fedha ili barabara hiyo iweze kujengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Naibu Spika, na mara fedha itakapopatikana kama ambavyo imeainishwa basi katika mpango huu wa miaka mitano ni kati ya barabara ambazo ziko kwenye mpango wa kujengwa kwa kiwango cha lami. Ahsante.

Name

Cecil David Mwambe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ndanda

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Katesh – Hydom kwa kiwango cha lami ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za afya katika Hospitali ya Hydom pamoja na usafirishaji wa mazao hasa ngano?

Supplementary Question 3

MHE. CECIL D. MWAMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza kwenye Wizara ya Ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wakazi wa Mtwara, Lindi pamoja na Ruvuma tunalazimika kufika Dar es Salaam kabla ya kuja Dodoma ambako ndiko Makao Makuu ya nchi. Lakini kimsingi kuna barabara inayoanzia Songea barabara nyingine inaanzia Masasi, Nachingwea, Liwale, Lupilo inakuja kutokea Morogoro, Ifakara, Malinyi ili kuweza kufika Dodoma kirahisi badala ya kutulazimisha tufike kwanza Dar es Salaam ndipo tuje Dodoma.

Sasa swali langu kwa Serikali kutokana na umuhimu wa barabara hii kwa watu wa mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma ili tuweze kufika kirahisi Makao Makuu ya nchi ambako ni Dodoma, ni lini itatengenezwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG.
GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Cecil Mwambe, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli barabara anayoitaja ni barabara kuu; siyo barabara ya mkoa, ni barabara kuu, ambayo kama nimemuelewa ni hii barabara ambayo inaoanzia Lumecha, Londo, Kilosa kwa Mpepo, Malinyi, Ifakara hadi Mikumi ambayo nadhani inaunganisha mikoa ya Mtwara, Lindi na Songea kuja Makao Makuu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara hii iko kwenye mpango, na kama ameangalia bajeti tayari, na baadhi ya maeneo kuanzia tumejenga Daraja lile la Magufuli pale Mto Kilombero lakini pia kuna kipande cha lami ambacho kinajengwa kati ya Kidatu kuja Ifakara, na sasa ipo kwenye mpango kwa ajili ya kuendelea na barabara kuanzia Lupilo kwenda huku Kilosa kwa Mpepo hadi kuunganisha huku Songea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachotakiwa tu ni fedha kupatikana halafu tukamilishe hiyo barabara kuu ambayo kwa kweli imekuwa ni hitaji kubwa sana kwa wananchi na Wabunge wa mikoa ya kusini ambayo ni ya Ruvuma, Mtwara, Lindi na Morogoro yenyewe. Ahsante.