Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 427 2021-06-15

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya Katesh – Hydom kwa kiwango cha lami ili kuwarahisishia wananchi kupata huduma za afya katika Hospitali ya Hydom pamoja na usafirishaji wa mazao hasa ngano?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi naomba kujibu swali la Mheshimiwa Samweli Xaday Hhayuma, Mbunge wa Hanang, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Barabara ya Katesh – Hydom yenye urefu wa kilometa 67 ni sehemu ya barabara ya mchepuo wa Mbuga ya Serengeti (Serengeti Southern Bypass) ambayo inahudumiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS).

Mheshimiwa Mwenyekiti, kazi ya upembuzi yakinifu wa Barabara ya Mchepuo ya Mbuga ya Serengeti (Serengeti Southern Bypass) yenye urefu wa kilometa 575.6 inayojumuisha barabara ya Karatu – Hydom – Lalago hadi Maswa yenye kilometa 446.6, Katesh – Hydom yenye kilometa 67 na Kolandoto – Lalago yenye kilometa 62 inatekelezwa kwa ufadhili wa Benki ya Ujerumani. Upembuzi yakinifu unatarajiwa kukamilika mwezi Juni, mwaka huu 2021. Ujenzi kwa kiwango cha lami wa barabara ya Katesh – Hydom utaanza pindi usanifu wa kina utakapokamilika na kadri ya upatikanaji wa fedha. Ahsante.