Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya kufikisha umeme wa msongo mkubwa katika Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, nashukuru pia kwa majibu mazuri ya Serikali yanayotia moyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sura ilivyo katika eneo la mradi kuna hali ya kusuasua, nilichokuwa naomba nafahamu uhakiki wa uwezo wa mtengenezaji kwa maana ya due- diligence jambo hili bado halijafanyika sambamba na utiaji saini mikabata, nilikuwa naiomba Serikali inihakikishie ni lini suala hili litafanyika ili kuharakisha mradi huu? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kapufi wa Mpanda kama ifuatavyo, kama tulivyosema katika swali la msingi ni kwamba tayari ujenzi umeanza kwenye maeneo hayo na vituo vya kupoozea umeme tayari vimetengenezwa na majengo yake yamekamilika kwa asilimia 90, ni kweli kwamba uhakiki wa uwezo wa Mkandarasi wa kututengenezea vile vifaa vya ndani ya kile chumba cha kupoozea umeme vikiwemo generator, transforma na vitu kama hivyo broker na breakers nyingine haujafanyika vizuri kwasababu ya tatizo kubwa ambalo liliwapata wenzetu ambao wanaweze kututengenezea vifaa hivi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, imekuwa ni vigumu kwetu sisi kutuma wataalam wetu kwenda kwenye hizo nchi ambazo zinao watengenezaji wa vifaa hivi vikubwa kwenda kuhakiki uwezo wa watengenezaji hao. Lakini nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ufuatiliaji wake sisi kwetu ni faraja na tunaelekea kukamilisha kwa sababu tayari sasa nchi ambazo zinatengeneza vifaa hivi zimeanza kuruhusu watu mbalimbali kwenda kufanya shughuli mbalimbali kwenye nchi zao baada ya janga la Korona kupungua kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunajiandaa kutuma wataalam wetu kwenda kuhakiki kama wale tuliowapa kazi wana uwezo wa kutengeneza hizo mashine tunazoziomba na baada ya hapo mikataba itasainiwa kama tulivyosema kwenye jibu la Msingi kwamba 2023 mradi huu utakuwa umekamilika na grid ya Taifa itafika Mpanda.

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya kufikisha umeme wa msongo mkubwa katika Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 2

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, toka mradi wa REA-I na REA- II katika Wilaya ya Kyela Vijiji vya Lupaso Ndondwa na Mabuga mpaka sasa hawajapata umeme.

Je, nini jitihada za Serikali kuhakikisha tunapata umeme maeneo hayo. Ahsante.

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mwakagenda Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli yapo baadhi ya maeneo ambayo REA I na REA II ilikuwa haijakamillisha, kulikuwa na changamoto mbalimbali ambazo sasa tumezitafutia mkakati maalum wa kuzimaliza na tunahakikisha kwamba inapoelekea 2022 tunapomaliza REA III round II na vile viporo vyote vya nyuma tutakuwa tumevimaliza, yalikuwepo matatizo ya Wakandarasi kushindwa kumalizia kazi kwa sababu ya changamoto mbalimbali lakini sasa tatizo hilo tumelitibu na tutahakikisha kwamba kila mwananchi anapata umeme katika maeneo yote ambayo yamepitiwa na mradi kulingana na scope ilivyokuwa kufikia 2022 kama ambavyo tumesema.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya kufikisha umeme wa msongo mkubwa katika Mkoa wa Katavi?

Supplementary Question 3

MHE. DAVID M. KIHENZILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa fursa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali hili la hali ya Mufindi linafanana pia na hapa mtangulizi amezungumza lakini tofauti ni kwamba asilimia 70 ya nguzo katika nchi hii zinatoka pale kwenye Jimbo letu, sasa ni lini Serikali itapeleka umeme kwenye maeneo ambayo ni ya giza pamoja na kwamba nguzo zinatoka pale, especial maeneo la Idete, Maduma pamoja na Idunda na vijiji vya Kisasa na maeneo mengine ambayo hayana umeme kabisa na wanashuhudia nguzo zikipita kila siku mbele yao. (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimwa Kihenzile Mbunge wa Mufindi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba tunakiri kuna maeneo bado hayana umeme mpaka sasa, Mufindi ni eneo mojawapo ambalo mkandarasi wa REA III round II tayari amepatikana MS Servicies na tayari ameenda kufanya survey kwenye maeneo husika, tunamhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba utuatiliaji wake ambao amekuwa akiufanya mara kwa mara utazaa matunda na tutapeleka umeme katika vijiji vyote alivyovisema.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo hilo lazima lipewe kipaumbele na heshima kwa sababu ndiyo linalisha na maeneo mengine yanayotumia nguzo za miti, kwa hiyo kweli katika hali ya kawaida siyo kitu cha kufurahisha kuona unatoa bidhaa halafu wewe haunufaiki nayo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba kabla ya mwaka 2022 kukamilika tutakuwa tayari tumefikisha umeme katika maeneo yote ambayo hayana umeme. (Makofi)