Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 3 Sitting 51 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 424 2021-06-15

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya kufikisha umeme wa msongo mkubwa katika Mkoa wa Katavi?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nishati, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sebastian Simon Kapufi, Mbunge wa Mpanda Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inaendelea na utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa njia kuu ya kusafirisha umeme wa gridi ya Taifa kwa msongo wa kilovolti 132 yenye urefu wa kilometa 381 kutoka Tabora hadi Katavi na ujenzi wa vituo vitatu vya kupoza umeme vya msongo wa kilovolti 132 kwenda 133 vya Ipole, Inyonga na Mpanda. Ujenzi wa majengo ya vituo vya kupooza umeme vya Ipole na Inyonga pamoja na uzio umekamilika kwa takribani asilimia 90. Mradi unatarajia kukamilika ifikapo Agosti, 2023, gharama ya mradi ni Shilingi Bilioni 64.9.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali pia inaendelea na utaratibu wa ujenzi wa njia kuu ya kusafirisha umeme mkubwa wa kilovoti 400 kutoka Iringa, Mbeya, Tunduma, Sumbawanga kupitia Mpanda hadi Kigoma takribani kilometa 1,232. Kazi inayofanyika kwa sasa ni kukamilisha taratibu za kupata Mtaalamu Mshauri wa kuandaa nyaraka za kumpata Mkandarasi wa kuanza ujenzi wa mradi. Ujenzi wa mradi unatarajiwa kuanza Novemba, 2022 na kukamilika mwezi Oktoba, 2024. Gharama ya mradi ni Shilingi Bilioni 470.42.