Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILVESTRY F. KOKA aliuliza:- Mradi wa kusambaza umeme katika Jimbo la Kibaha Mjini unakwenda kwa kusuasua:- Je, ni lini Mradi huo utakamilika ili Wananchi wa Kibaha Mjini waondokane na adha ya umeme?

Supplementary Question 1

MHE. SILYVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niipongeze Serikali kwa sababu kwa kweli kwa kipindi kifupi imefanya kazi nzuri na hasa ilivyoondoa mkanganyo wa ulipaji wa kufungiwa umeme kwa wananchi ili tunalishukuru sana Serikali yetu imefanya vizuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Jimbo la Kibaha bado tuna matatizo makubwa ya kusambaziwa umeme kwa wananchi na hususani katika mitaa ya Viziwaziwa kwa maana ya Sagale Magengeni, Sagale kambini lakini Muheza pamoja na maeneo mengine ya Misugusugu kwa maana ya Zogohale na Miomboni pia vilevile Madina hadi Kiembeni toka 2016 baadhi ya wananchi bado hawajapata umeme.

Je, ni lini sasa wananchi hawa watawekewa umeme ili waondokane na adha ya kukosa umeme katika Mji wa Kibaha?

Swali la pili, toka mwaka 2014 wananchi wengi wa Jimbo la Kibaha mjini walisimamishiwa maendeleo katika maeneo yao ambayo kunategemewa kupita mradi wa umeme wa msongo wa Kilowatt 400 kutoka Kinyerezi kuelekea Chalinze wasifanye lolote ingawa hadi leo bado wengine wanaendelea hata kutozwa kodi za ardhi.

Je, ni lini wananchi hawa watapata fidia zao ili waweze kufanya maendeleo maeneo mengine na kuondokana na adha hii?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Koka Mbunge wa Kibaha kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba baadhi ya maeneo ya Mji wetu wa Kibaha hayajapata umeme lakini tayari Serikali imejitahidi kupeleka umeme katika hayo maeneo machache ambayo ni jitihada ya Mheshimiwa Mbunge katika kufanya ufuatiliaji wa kina kuhakikisha maeneo yote yanapata umeme. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba maeneo yote ya Kibaha yataendelea kupelekewa umeme kupitia mradi wetu wa Peri- Urban na tayari Mkandarasi huyo ameshaongezewa scope ya kazi kwa hiyo maeneo yote ya Ziwaziwa na mengine ambayo yametajwa na Mheshimiwa Mbunge yote yatafikiwa na umeme kadri tunavyozidi kuendelea mbele kwasababau ni jukumu la TANESCO na REA na Serikali kuendelea kupeleka umeme kwa wananchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye swali la pili, ni kweli kwamba kuna maeneo ambayo yalitwaliwa na Serikali kwa nia ya kupitisha mradi wa Msongo wa kilovolti 400 kusafirisha umeme na sasa utakuwa unasafirishwa kutoka Chalinze kuelekea Kinyelezi kwa sababu uzalishaji mkubwa unafanyika katika maeneo ya Mwalimu Nyerere.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali tayari imetoa fedha kwa TANESCO takribani Billioni 29.6 na kuanzia Julai, Mosi fidia zitaanza kulipwa kwa wananchi wa maeneo ya Chalinze, maeneo ya Kibaha na maeneo ya Kinyerezi kwa ajili ya kupisha mradi huo uanze kujengwa mara moja.